Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 34:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 anayehifadhi fadhili zenye upendo kwa ajili ya maelfu,+ anayesamehe kosa na ubaya na dhambi,+ lakini kwa vyovyote hatakosa kuadhibu,+ anayeleta adhabu kwa ajili ya kosa la akina baba juu ya wana na juu ya wajukuu, juu ya kizazi cha tatu na juu ya kizazi cha nne.”+

  • Nehemia 9:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kwa hiyo wakakataa kusikiliza,+ wala hawakuyakumbuka+ matendo yako ya ajabu ambayo ulikuwa umewafanyia, bali wakafanya shingo zao kuwa ngumu+ na kujichagulia mkuu+ ili kurudi kwenye hali yao ya utumwa katika Misri. Lakini wewe ni Mungu wa matendo ya kusamehe,+ mwenye neema+ na rehema,+ si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi+ wa fadhili zenye upendo, nawe hukuwaacha.+

  • Zaburi 65:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Mambo yenye makosa yamekuwa na nguvu kuliko mimi.+

      Nayo makosa yetu, wewe mwenyewe utayafunika.+

  • Zaburi 86:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni mwema+ na uko tayari kusamehe;+

      Na fadhili zenye upendo ni nyingi kwa wale wote wanaokuitia.+

  • Isaya 1:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Sasa, njooni, nasi tunyooshe mambo kati yetu,” asema Yehova.+ “Hata dhambi zenu zikiwa nyekundu, zitafanywa kuwa nyeupe kama theluji;+ hata zikiwa nyekundu kama kitambaa chekundu; zitakuwa kama sufu.

  • Isaya 44:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Nitayafutilia mbali makosa yako kana kwamba ni kwa wingu,+ na dhambi zako kana kwamba ni kwa wingu kubwa. Rudi kwangu,+ kwa maana nitakukomboa.+

  • Yeremia 50:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 “Na katika siku hizo na katika wakati huo,”+ asema Yehova, “kosa la Israeli litatafutwa,+ lakini halitakuwapo; na dhambi za Yuda,+ nazo hazitapatikana, kwa maana nitawasamehe wale nitakaowaacha wabaki.”+

  • Danieli 9:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Kwake Yehova Mungu wetu, kuna rehema+ na msamaha,+ kwa maana tumemwasi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki