32 Kwa mfano, yeyote yule anayesema neno baya juu ya Mwana wa binadamu, atasamehewa;+ lakini yeyote yule anayesema vibaya juu ya roho takatifu, hilo hatasamehewa, hapana, si katika mfumo huu wa mambo wala katika ule utakaokuja.+
4 Kwa maana haiwezekani kamwe kwa habari ya wale ambao wametiwa nuru+ mara moja kwa wakati wote, na ambao wameonja zawadi ya bure+ ya kimbingu, na ambao wamekuwa washiriki wa roho takatifu,+
6 lakini ambao wameanguka,+ kuwarudisha tena kwenye toba,+ kwa sababu wanamtundika upya mtini Mwana wa Mungu kwa ajili yao wenyewe na kumfunua yeye kwenye aibu ya hadharani.+
26 Kwa maana tukizoea kutenda dhambi kimakusudi+ baada ya kupokea ujuzi sahihi juu ya kweli,+ hakuna tena dhabihu yoyote iliyobaki kwa ajili ya dhambi,+
16 Yeyote akimwona ndugu yake anafanya dhambi, dhambi ambayo haileti kifo,+ yeye ataomba, naye atampa huyo uzima,+ ndiyo, kwa wale ambao hawafanyi dhambi inayoleta kifo.+ Kuna dhambi ambayo huleta kifo. Ni kuhusu dhambi hiyo kwamba simwambii aombe.+