Zaburi
Muziki wa Asafu.
79 Ee Mungu, mataifa yameingia katika urithi wako;+
Wamelitia unajisi hekalu lako takatifu;+
Wamefanya Yerusalemu kuwa rundo la mabomoko.+
2 Wamewapa ndege wa mbinguni maiti ya watumishi wako iwe chakula chao,+
Na nyama ya washikamanifu wako kwa wanyama-mwitu wa dunia.+
5 Ee Yehova, utapandwa na hasira mpaka wakati gani? Milele?+
Hasira yako itawaka kama moto mpaka wakati gani?+
6 Mwaga ghadhabu yako juu ya mataifa ambayo hayakukujua,+
Na juu ya falme ambazo hazikuliitia jina lako.+
8 Usikumbuke dhidi yetu makosa ya mababu zetu.+
Ufanye haraka! Rehema zako na zitufikie,+
Kwa maana tumekuwa maskini sana.+
9 Utusaidie, Ee Mungu wa wokovu wetu,+
Kwa ajili ya utukufu wa jina lako;+
Na utukomboe na kufunika dhambi zetu kwa sababu ya jina lako.+
10 Kwa nini mataifa yaseme: “Mungu wao yuko wapi?”+
Na ijulikane katika mataifa mbele ya macho yetu+
Juu ya kulipiza kisasi damu ya watumishi wako ambayo imemwagwa.+
11 Kuugua kwa mfungwa na kuingie mbele zako.+
Kulingana na ukuu wa mkono wako, uwahifadhi wale waliochaguliwa kwa ajili ya kifo.+