Zaburi
Muziki wa Daudi.
143 Ee Yehova, uisikie sala yangu;+
Utege sikio usikie kusihi kwangu.+
Katika uaminifu wako unijibu kwa uadilifu wako.+
2 Wala usiingie katika hukumu pamoja na mtumishi wako;+
Kwa maana mbele zako, hakuna yeyote aliye hai anayeweza kuwa mwadilifu.+
3 Kwa maana adui ameifuatilia nafsi yangu;+
Ameuponda uhai wangu mpaka chini.+
Amenifanya nikae katika mahali penye giza kama wale waliokufa kwa wakati usio na kipimo.+
5 Nimezikumbuka siku za zamani za kale;+
Nimetafakari juu ya utendaji wako wote;+
Kwa kupenda niliendelea kuhangaikia kazi ya mikono yako mwenyewe.+
7 Ufanye haraka, unijibu, Ee Yehova.+
Roho yangu imefikia mwisho.+
Usiufiche uso wako mbali nami,+
Kama sivyo nitakuwa kama wale wanaoshuka kuingia shimoni.+
8 Asubuhi unifanye nisikie fadhili zako zenye upendo,+
Kwa maana nimekutegemea wewe.+
Unijulishe njia ninayopaswa kuitembea,+
Kwa maana nimekuinulia nafsi yangu.+
10 Unifundishe kufanya mapenzi yako,+
Kwa maana wewe ni Mungu wangu.+
Roho yako ni nzuri;+
Na iniongoze katika nchi ya unyoofu.+