Wagalatia
Kwa Wagalatia
1 Paulo,+ mtume,+ si kutokana na wanadamu wala kupitia mwanadamu fulani, bali kupitia Yesu Kristo+ na Mungu Baba,+ aliyemfufua yeye kutoka kwa wafu,+ 2 na ndugu wote walio pamoja nami,+ kwa makutaniko ya Galatia:+
3 Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani+ kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo. 4 Alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu+ ili atukomboe kutoka katika mfumo mwovu wa mambo+ wa sasa, kulingana na mapenzi+ ya Mungu na Baba yetu, 5 kwake kuwe na utukufu milele na milele.+ Amina.
6 Mimi ninashangaa kwamba mnaondolewa upesi hivyo kutoka kwake Yeye+ aliyewaita ninyi kwa fadhili zisizostahiliwa+ za Kristo nanyi mnapelekwa kwenye habari njema ya aina nyingine.+ 7 Lakini si nyingine; isipokuwa tu kuna watu fulani wanaowataabisha+ ninyi na kutaka kupotosha habari njema juu ya Kristo.+ 8 Lakini, hata ikiwa sisi au malaika kutoka mbinguni tungewatangazia ninyi kuwa habari njema jambo fulani kupita lile tulilowatangazia ninyi kuwa habari njema, mtu huyo na alaaniwe.+ 9 Kama vile tulivyosema hapo juu, sasa mimi pia nasema tena, Mtu yeyote anayewatangazia ninyi jambo fulani kupita lile mlilopokea+ kuwa hilo ni habari njema, na alaaniwe.
10 Kwa kweli, je, sasa ninajaribu kushawishi wanadamu au Mungu? Au je, ninatafuta kuwapendeza wanadamu?+ Kama ningekuwa bado ninawapendeza wanadamu,+ mimi singekuwa mtumwa+ wa Kristo. 11 Kwa maana nawajulisha ninyi, akina ndugu, kwamba habari njema ambayo niliitangaza kuwa habari njema si jambo la kibinadamu;+ 12 kwa maana sikuipokea kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa hiyo, isipokuwa kupitia ufunuo wa Yesu Kristo.+
13 Bila shaka, ninyi mlisikia juu ya mwenendo wangu hapo zamani katika dini ya Kiyahudi,+ kwamba kufikia hatua ya kuzidi mno niliendelea kulitesa+ kutaniko la Mungu na kuliangamiza,+ 14 nami nilikuwa nikifanya maendeleo makubwa zaidi katika dini ya Kiyahudi kuliko watu wengi wa umri wangu katika jamii yangu,+ kwa kuwa nilikuwa mwenye bidii zaidi+ kwa ajili ya mapokeo+ ya baba zangu. 15 Lakini wakati Mungu, aliyenitenga mimi tangu tumbo la uzazi la mama yangu na kuniita+ kupitia fadhili zake zisizostahiliwa,+ alipoona vema 16 kumfunua Mwana wake kuhusiana nami,+ ili nitangaze habari njema juu yake kwa mataifa,+ mimi sikuingia mara moja katika mashauriano pamoja na watu wenye mwili na damu.+ 17 Wala sikupanda kwenda Yerusalemu kwa wale waliokuwa mitume kabla yangu,+ bali nilienda nikaingia Arabia, nami nikarudi tena Damasko.+
18 Kisha miaka mitatu baadaye nilipanda kwenda Yerusalemu+ kumtembelea Kefa,+ nami nikakaa pamoja naye siku kumi na tano. 19 Lakini sikuona mwingine yeyote wa wale mitume, isipokuwa Yakobo+ ndugu+ ya Bwana. 20 Sasa kuhusu mambo ninayowaandikia ninyi, tazameni! machoni pa Mungu, mimi sisemi uwongo.+
21 Baada ya hayo nilienda+ katika maeneo ya Siria na ya Kilikia. 22 Lakini mimi sikujulikana kwa uso kwa makutaniko ya Yudea yaliyokuwa katika muungano na Kristo;+ 23 yalikuwa tu yakisikia: “Yule mtu ambaye hapo zamani alitutesa+ sasa anaitangaza habari njema juu ya imani ambayo hapo zamani aliiangamiza.”+ 24 Kwa hiyo wakaanza kumtukuza+ Mungu kwa sababu yangu.