2 Wathesalonike
3 Mwishowe, akina ndugu, endeleeni kusali kwa ajili yetu,+ ili neno la Yehova+ liendelee kusonga haraka+ na kutukuzwa kama vile linavyofanya kwenu; 2 na ili tukombolewe kutoka kwa watu wenye madhara na waovu,+ kwa maana imani si mali ya watu wote.+ 3 Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawafanya ninyi kuwa imara na kuwaepusha na yule mwovu.+ 4 Zaidi ya hayo, tuna uhakika+ katika Bwana kuwahusu ninyi, kwamba mnafanya nanyi mtaendelea kufanya mambo tunayoagiza.+ 5 Bwana na aendelee kuielekeza mioyo yenu kwa mafanikio katika kumpenda+ Mungu na katika uvumilivu+ kwa ajili ya Kristo.
6 Sasa tunawapa ninyi maagizo,+ akina ndugu, katika jina la Bwana Yesu Kristo, mjiepushe+ na kila ndugu anayetembea bila utaratibu+ na si kulingana na pokeo mlilopokea kutoka kwetu.+ 7 Kwa maana ninyi wenyewe mnajua njia mnayopaswa kutuiga,+ kwa sababu hatukujiendesha bila utaratibu katikati yenu+ 8 wala hatukula chakula kwa yeyote bure.+ Kinyume cha hilo, kwa kazi ya jasho na kutaabika+ usiku na mchana tulikuwa tukifanya kazi ili tusimtwike yeyote kati yenu mzigo wenye gharama.+ 9 Si kwamba hatuna mamlaka,+ bali ili tujitoe kuwa kielelezo kwenu ili mtuige sisi.+ 10 Kwa kweli, pia, tulipokuwa pamoja nanyi, tulikuwa tukiwapa ninyi agizo hili:+ “Ikiwa yeyote hataki kufanya kazi, basi na asile chakula.”+ 11 Kwa maana tunasikia watu fulani wanatembea bila utaratibu+ katikati yenu, hawafanyi kazi hata kidogo bali wanajiingiza katika mambo yasiyowahusu wao.+ 12 Kwa watu wa namna hiyo tunawapa agizo na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo kwamba kwa kufanya kazi kwa utulivu wale chakula ambacho wao wenyewe wanafanyia kazi.+
13 Kwa upande wenu, akina ndugu, msiache kutenda yaliyo sawa.+ 14 Lakini ikiwa yeyote hatii neno letu+ kupitia barua hii, mtieni alama mtu huyo,+ acheni kushirikiana naye,+ ili aone aibu.+ 15 Na bado msimwone yeye kuwa adui, bali endeleeni kumwonya+ kama ndugu.
16 Sasa Bwana wa amani mwenyewe na awape ninyi amani daima katika kila njia.+ Bwana na awe pamoja nanyi nyote.
17 Hii ni salamu yangu, ya Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe,+ ambayo ni ishara katika kila barua; hivi ndivyo mimi huandika.
18 Fadhili zisizostahiliwa+ za Bwana wetu Yesu Kristo na ziwe pamoja nanyi nyote.