Zaburi
Maskili. Ya Daudi, alipokuwa pangoni.+ Sala.
142 Kwa sauti yangu, nilimwomba Yehova msaada;+
Kwa sauti yangu, nilianza kumlilia Yehova anionyeshe kibali.+
2 Mbele zake niliendelea kumwaga hangaiko langu;+
Mbele zake niliendelea kutangaza juu ya taabu yangu mwenyewe,+
3 Roho+ yangu ilipozimia ndani yangu.
Ndipo wewe mwenyewe ulipoijua barabara yangu.+
Katika njia ambayo mimi hutembea+
Wametega mtego kwa ajili yangu.+
4 Tazama kwenye mkono wa kuume uone
Kwamba hakuna yeyote anayenitambua mimi.+
Mahali pangu pa kukimbilia pameangamia;+
Hakuna yeyote anayeuliza habari za nafsi yangu.+