2 Wakorintho
6 Huku tukifanya kazi pamoja naye,+ tunawasihi ninyi pia msipokee fadhili zisizostahiliwa za Mungu kisha mkose kusudi lake.+ 2 Kwa maana anasema: “Katika wakati unaokubalika nilikusikia, na katika siku ya wokovu nilikusaidia.”+ Tazama! Sasa ndio wakati unaokubalika+ hasa. Tazama! Sasa ndiyo siku ya wokovu.+
3 Sisi hatutoi sababu yoyote ya kukwaza+ kwa njia yoyote, ili huduma yetu isilaumiwe;+ 4 bali katika kila njia tunajipendekeza+ kuwa wahudumu wa Mungu, kwa kuvumilia mengi, kwa dhiki, kwa hali za uhitaji, kwa magumu,+ 5 kwa mapigo, kwa vifungo vya gerezani,+ kwa machafuko, kwa kazi za jasho, kwa kukosa usingizi usiku, kwa nyakati za kuwa bila chakula,+ 6 kwa utakato, kwa ujuzi, kwa ustahimilivu,+ kwa fadhili,+ kwa roho takatifu, kwa upendo usio na unafiki,+ 7 kwa kusema maneno ya kweli, kwa nguvu za Mungu;+ kupitia silaha+ za uadilifu upande wa mkono wa kuume na wa kushoto, 8 kupitia utukufu na aibu, kupitia habari ambazo ni mbaya na habari ambazo ni njema; kama wanaodanganya+ na bado ni wenye kusema kweli, 9 kama wasiojulikana na bado ni wenye kutambuliwa,+ kama wanaokufa na bado, tazama! tunaishi,+ kama wanaotiwa nidhamu+ na bado hatukabidhiwi kwenye kifo,+ 10 kama walio na huzuni lakini wenye kushangilia sikuzote, kama maskini lakini wenye kuwatajirisha wengi, kama wasio na kitu chochote na bado wenye kuwa na vitu vyote.+
11 Kinywa chetu kimefunguliwa kwenu, enyi Wakorintho, moyo+ wetu umepanuka. 12 Ninyi hamjasongwa mkakosa nafasi ndani yetu,+ lakini mmesongwa mkakosa nafasi katika upendo wenu mwororo.+ 13 Kwa hiyo, yakiwa kama malipo—mimi nasema kana kwamba ni kwa watoto+—ninyi, pia, panukeni.
14 Msifungwe nira isivyo sawa pamoja na wasio waamini.+ Kwa maana kuna ushirika gani kati ya uadilifu na uasi-sheria?+ Au nuru ina ushirika gani na giza?+ 15 Na zaidi, kuna upatano gani kati ya Kristo na Beliali?+ Au mtu mwaminifu ana fungu+ gani na asiye mwamini? 16 Na hekalu la Mungu lina upatano gani na sanamu?+ Kwa maana sisi ni hekalu+ la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema: “Mimi nitakaa katikati yao+ na kutembea katikati yao, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”+ 17 “ ‘Kwa hiyo tokeni katikati yao, na mjitenge,’ asema Yehova, ‘na mwache kugusa kitu kilicho najisi’ ”;+ “ ‘nami nitawakaribisha ndani.’ ”+ 18 “ ‘Nami nitakuwa baba kwenu,+ nanyi mtakuwa wana na mabinti kwangu,’+ asema Yehova Mweza-Yote.”+