Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 24:14, 15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Akawapeleka uhamishoni watu wote wa Yerusalemu, wakuu wote,+ mashujaa wote hodari, na kila fundi na mfua chuma*+—aliwapeleka uhamishoni watu 10,000. Hakuna yeyote aliyebaki isipokuwa watu maskini kabisa nchini.+ 15 Basi akampeleka Yehoyakini+ uhamishoni Babiloni;+ alimpeleka pia mama ya mfalme, wake za mfalme, maofisa wa makao yake, na viongozi wa nchi, akawapeleka uhamishoni Babiloni kutoka Yerusalemu.

  • 1 Mambo ya Nyakati 3:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Wana wa Yehoyakimu walikuwa Yekonia+ mwanawe na Sedekia mwana wa Yekonia.

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Yehoyakini+ alikuwa na umri wa miaka 18 alipoanza kutawala, alitawala kwa miezi mitatu na siku kumi huko Yerusalemu; naye aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova.+ 10 Mwanzoni mwa mwaka,* Mfalme Nebukadneza aliagiza aletwe Babiloni,+ pamoja na vyombo vyenye thamani vya nyumba ya Yehova.+ Akamweka Sedekia ndugu ya baba yake kuwa mfalme wa Yuda na Yerusalemu.+

  • Yeremia 22:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Je, mtu huyu Konia ni chungu tu kilichodharauliwa na kuvunjika,

      Chombo ambacho hakuna mtu anayekitaka?

      Kwa nini yeye na wazao wake wameangushwa chini

      Na kutupwa katika nchi wasiyoijua?’+

  • Yeremia 24:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Kisha Yehova akanionyesha vikapu viwili vya tini vilivyowekwa mbele ya hekalu la Yehova, baada ya Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni kumpeleka uhamishoni Yekonia*+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, pamoja na wakuu wa Yuda, mafundi, na wahunzi;* aliwatoa Yerusalemu na kuwapeleka Babiloni.+

  • Yeremia 37:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 37 Na Mfalme Sedekia+ mwana wa Yosia akaanza kutawala baada ya Konia*+ mwana wa Yehoyakimu, kwa maana Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni alikuwa amemweka kuwa mfalme katika nchi ya Yuda.+

  • Yeremia 52:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Kisha katika mwaka wa 37 tangu Mfalme Yehoyakini+ wa Yuda alipopelekwa uhamishoni, katika mwezi wa 12, siku ya 25 ya mwezi huo, Mfalme Evil-merodaki wa Babiloni, katika mwaka alioanza kutawala, alimwachilia huru Mfalme Yehoyakini wa Yuda na kumtoa gerezani.+

  • Mathayo 1:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Yosia+ akawa baba ya Yekonia+ na ndugu zake, wakati wa kupelekwa uhamishoni Babiloni.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki