Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 126:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 126 Yehova alipowakusanya na kuwarudisha mateka wa Sayuni,+

      Tulifikiri tunaota ndoto.

  • Yeremia 23:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 “Kisha nitawakusanya kondoo wangu waliobaki kutoka katika nchi zote ambako nilikuwa nimewatawanya,+ nami nitawarudisha kwenye malisho yao,+ nao watazaana na kuwa wengi.+

  • Ezekieli 39:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitawarudisha watu wa Yakobo waliotekwa+ na kuwaonyesha rehema watu wote wa nyumba ya Israeli;+ nami nitalitetea jina langu takatifu kwa bidii.*+

  • Amosi 9:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Nitawakusanya na kuwarudisha watu wangu Waisraeli walio utekwani,+

      Nao watajenga upya majiji yaliyoachwa ukiwa na kuishi humo;+

      Watapanda mashamba ya mizabibu na kunywa divai yake,+

      Nao watalima bustani za matunda na kula matunda yake.’+

  • Mika 2:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kwa hakika nitawakusanya ninyi nyote, enyi watu wa Yakobo;

      Kwa kweli nitawakusanya pamoja wale wanaobaki wa Israeli.+

      Kwa umoja nitawaweka kama kondoo zizini,

      Kama kundi la kondoo katika malisho yake;+

      Litakuwa na kelele za watu.’+

  • Mika 4:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Gaagaa na kulia kwa uchungu, Ee binti ya Sayuni,

      Kama mwanamke anayezaa,

      Kwa maana sasa utatoka jijini na kuishi shambani.

      Utaenda mpaka Babiloni,+

      Na huko utaokolewa;+

      Huko Yehova atakununua tena kutoka mikononi mwa maadui wako.+

  • Sefania 3:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Wakati huo nitawaleta ndani,

      Wakati nitakapowakusanya pamoja.

      Kwa maana nitawafanya kuwa kitu cha umaarufu* na sifa+ miongoni mwa mataifa yote duniani,

      Nitakapowakusanya mateka wenu mbele ya macho yenu,” asema Yehova.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki