97 Yehova amekuwa Mfalme!+
Dunia na iwe na shangwe.+
Na visiwa vyake vingi vishangilie.+
 2 Mawingu na giza zito vinamzunguka;+
Uadilifu na haki ndio msingi wa kiti chake cha ufalme.+
 3 Moto hutangulia mbele zake+
Na kuwateketeza kabisa maadui wake pande zote.+
 4 Umeme wake wa radi huiangazia nchi;
Dunia huona na kutetemeka.+
 5 Milima huyeyuka kama nta mbele za Yehova,+
Mbele za Bwana wa dunia yote.
 6 Mbingu hutangaza uadilifu wake,
Na mataifa yote huona utukufu wake.+
 7 Wote wanaoabudu sanamu yoyote ya kuchongwa na waaibishwe,+
Wale wanaojigamba kuhusu miungu yao ya ubatili.+
Mwinamieni, enyi miungu yote.+
 8 Sayuni husikia na kufurahi;+
Miji ya Yuda ina shangwe
Kwa sababu ya hukumu zako, Ee Yehova.+
 9 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote;
Umekwezwa juu zaidi ya miungu mingine yote.+
10 Enyi mnaompenda Yehova, chukieni maovu.+
Anaulinda uhai wa washikamanifu wake;+
Huwaokoa kutoka katika mkono wa mwovu.+
11 Nuru imemwangazia mwadilifu+
Na shangwe walio wanyoofu moyoni.
12 Shangilieni kwa sababu ya Yehova, enyi waadilifu,
Na mlishukuru jina lake takatifu.