Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 25
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

2 Mambo ya Nyakati—Yaliyomo

      • Amazia, mfalme wa Yuda (1-4)

      • Apigana vita na Edomu (5-13)

      • Amazia aabudu sanamu (14-16)

      • Apigana vita na Mfalme Yehoashi wa Israeli (17-24)

      • Kifo cha Amazia (25-28)

2 Mambo ya Nyakati 25:1

Marejeo

  • +2Fa 14:1-6

2 Mambo ya Nyakati 25:3

Marejeo

  • +2Nya 24:26

2 Mambo ya Nyakati 25:4

Marejeo

  • +Kum 24:16

2 Mambo ya Nyakati 25:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, ukoo wa upande wa baba.

  • *

    Tnn., “waliochaguliwa.”

Marejeo

  • +1Sa 8:11, 12
  • +Hes 1:2, 3

2 Mambo ya Nyakati 25:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.

2 Mambo ya Nyakati 25:7

Marejeo

  • +2Nya 19:2

2 Mambo ya Nyakati 25:8

Marejeo

  • +2Nya 14:11; 20:6

2 Mambo ya Nyakati 25:9

Marejeo

  • +1Sa 2:7; Met 10:22; Hag 2:8

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha,

    5/2023, uku. 7

2 Mambo ya Nyakati 25:11

Marejeo

  • +2Sa 8:13; Zb 60:utangulizi
  • +2Fa 14:7; 2Nya 20:10, 11

2 Mambo ya Nyakati 25:13

Marejeo

  • +2Nya 25:9
  • +1Fa 16:29
  • +2Nya 8:3, 5

2 Mambo ya Nyakati 25:14

Marejeo

  • +Kut 20:3, 5; Kum 7:25; 2Nya 28:22, 23

2 Mambo ya Nyakati 25:15

Marejeo

  • +2Nya 24:20; Zb 115:8; Yer 2:5; 10:5

2 Mambo ya Nyakati 25:16

Marejeo

  • +2Nya 16:10; 18:25, 26
  • +Isa 30:10
  • +1Sa 2:25; Met 29:1

2 Mambo ya Nyakati 25:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “tukutane uso kwa uso.”

Marejeo

  • +2Fa 14:8-10

2 Mambo ya Nyakati 25:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “jumba lako mwenyewe la kifalme.”

Marejeo

  • +2Nya 25:11

2 Mambo ya Nyakati 25:20

Marejeo

  • +2Fa 14:11-14
  • +2Nya 22:7
  • +2Nya 25:14

2 Mambo ya Nyakati 25:21

Marejeo

  • +Yos 21:8, 16; 1Sa 6:19

2 Mambo ya Nyakati 25:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “katika hema lake.”

2 Mambo ya Nyakati 25:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Anaitwa pia Ahazia.

  • *

    Karibu mita 178 (futi 584). Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Ne 8:16; 12:38, 39
  • +2Nya 26:9; Yer 31:38; Zek 14:10

2 Mambo ya Nyakati 25:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “jumba la.”

Marejeo

  • +1Fa 7:51; 15:18; 2Fa 24:12, 13; 25:13-15; 2Nya 12:9

2 Mambo ya Nyakati 25:25

Marejeo

  • +2Fa 14:1
  • +2Fa 13:10
  • +2Fa 14:17-20

2 Mambo ya Nyakati 25:27

Marejeo

  • +2Fa 12:20; 15:8, 10; 21:23

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

2 Nya. 25:12Fa 14:1-6
2 Nya. 25:32Nya 24:26
2 Nya. 25:4Kum 24:16
2 Nya. 25:51Sa 8:11, 12
2 Nya. 25:5Hes 1:2, 3
2 Nya. 25:72Nya 19:2
2 Nya. 25:82Nya 14:11; 20:6
2 Nya. 25:91Sa 2:7; Met 10:22; Hag 2:8
2 Nya. 25:112Sa 8:13; Zb 60:utangulizi
2 Nya. 25:112Fa 14:7; 2Nya 20:10, 11
2 Nya. 25:132Nya 25:9
2 Nya. 25:131Fa 16:29
2 Nya. 25:132Nya 8:3, 5
2 Nya. 25:14Kut 20:3, 5; Kum 7:25; 2Nya 28:22, 23
2 Nya. 25:152Nya 24:20; Zb 115:8; Yer 2:5; 10:5
2 Nya. 25:162Nya 16:10; 18:25, 26
2 Nya. 25:16Isa 30:10
2 Nya. 25:161Sa 2:25; Met 29:1
2 Nya. 25:172Fa 14:8-10
2 Nya. 25:192Nya 25:11
2 Nya. 25:202Fa 14:11-14
2 Nya. 25:202Nya 22:7
2 Nya. 25:202Nya 25:14
2 Nya. 25:21Yos 21:8, 16; 1Sa 6:19
2 Nya. 25:23Ne 8:16; 12:38, 39
2 Nya. 25:232Nya 26:9; Yer 31:38; Zek 14:10
2 Nya. 25:241Fa 7:51; 15:18; 2Fa 24:12, 13; 25:13-15; 2Nya 12:9
2 Nya. 25:252Fa 14:1
2 Nya. 25:252Fa 13:10
2 Nya. 25:252Fa 14:17-20
2 Nya. 25:272Fa 12:20; 15:8, 10; 21:23
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
2 Mambo ya Nyakati 25:1-28

Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati

25 Amazia alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 29 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Yehoadani wa Yerusalemu.+ 2 Aliendelea kutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova, lakini si kwa moyo kamili. 3 Mara tu ufalme ulipoimarika kabisa mikononi mwake, aliwaua watumishi wake waliomuua mfalme, baba yake.+ 4 Lakini hakuwaua wana wao, kwa maana alitenda kulingana na mambo yaliyoandikwa katika Sheria, katika kitabu cha Musa, ambamo Yehova aliamuru hivi: “Akina baba hawapaswi kuuawa kwa sababu ya wana wao, na wana hawapaswi kuuawa kwa sababu ya baba zao; lakini kila mtu anapaswa kuuawa kwa sababu ya dhambi yake mwenyewe.”+

5 Na Amazia akawakusanya pamoja watu wa Yuda na kuwaagiza wasimame kulingana na koo zao,* chini ya wakuu wa maelfu na chini ya wakuu wa mamia kwa ajili ya watu wote wa Yuda na Benjamini.+ Akawaandikisha waliokuwa na umri wa miaka 20 na zaidi,+ akapata kwamba walikuwa mashujaa 300,000 waliozoezwa* kwa ajili ya utumishi wa kijeshi, walioweza kutumia mkuki na ngao kubwa. 6 Isitoshe, alikodi mashujaa hodari 100,000 kutoka Israeli kwa talanta 100 za fedha.* 7 Lakini mtu fulani wa Mungu wa kweli akamjia na kumwambia: “Ee mfalme, usiruhusu jeshi la Israeli liende pamoja nawe, kwa maana Yehova hayuko pamoja na Waisraeli,+ hayuko pamoja na Mwefraimu yeyote. 8 Lakini nenda peke yako, utende, na uwe jasiri vitani. Usipofanya hivyo, Mungu wa kweli anaweza kukufanya ujikwae mbele ya adui, kwa maana Mungu ana nguvu za kusaidia+ na za kusababisha mtu ajikwae.” 9 Ndipo Amazia akamuuliza hivi mtu wa Mungu wa kweli: “Lakini vipi kuhusu zile talanta 100 ambazo nimewapa wanajeshi wa Israeli?” Mtu wa Mungu wa kweli akamjibu: “Yehova anaweza kukupa nyingi zaidi kuliko hizo.”+ 10 Basi Amazia akawaagiza wanajeshi waliokuwa wamekuja kwake kutoka Efraimu waende zao, warudi kwao. Hata hivyo, waliwakasirikia sana watu wa Yuda, basi wakarudi kwao wakiwa wamekasirika sana.

11 Kisha Amazia akajipa ujasiri na kuwaongoza wanajeshi wake mwenyewe kwenye Bonde la Chumvi,+ akawaua wanaume 10,000 wa Seiri.+ 12 Na wanaume wa Yuda wakawateka watu 10,000 wakiwa hai. Wakawapandisha juu ya mwamba na kuwatupa chini kutoka kwenye mwamba huo, na wote wakavunjika vipandevipande. 13 Lakini wanajeshi ambao Amazia aliwaambia warudi, wasiende pamoja naye vitani,+ walikuwa wakivamia majiji ya Yuda, kuanzia Samaria+ mpaka Beth-horoni;+ waliwaua watu 3,000 katika majiji hayo na kuchukua nyara nyingi sana.

14 Lakini Amazia aliporudi baada ya kuwaua Waedomu, alileta miungu ya watu wa Seiri na kuisimamisha ili iwe miungu yake mwenyewe,+ naye akaanza kuinama mbele ya miungu hiyo na kuifukizia moshi wa dhabihu. 15 Kwa hiyo Yehova akamkasirikia sana Amazia, akamtuma nabii ambaye alimwambia: “Kwa nini unaifuata miungu ya mataifa ambayo haikuwaokoa watu wake kutoka mikononi mwako?”+ 16 Nabii huyo alipokuwa akizungumza naye, mfalme akamwambia: “Je, tulikuweka uwe mshauri wa mfalme?+ Nyamaza!+ Kwa nini unataka kuuawa?” Ndipo nabii huyo akanyamaza, lakini akasema: “Najua kwamba Mungu ameamua kukuangamiza, kwa sababu umetenda hivyo na hujasikiliza ushauri wangu.”+

17 Baada ya kushauriana na washauri wake, Mfalme Amazia wa Yuda alituma ujumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mfalme wa Israeli akisema: “Njoo, tupambane vitani.”*+ 18 Mfalme Yehoashi wa Israeli akatuma ujumbe huu kwa Mfalme Amazia wa Yuda: “Gugu lenye miiba kule Lebanoni lilituma ujumbe huu kwa mwerezi huko Lebanoni, ‘Mpe mwanangu binti yako awe mke wake.’ Hata hivyo, mnyama wa mwituni wa Lebanoni akapita karibu na kulikanyaga-kanyaga gugu hilo lenye miiba. 19 Umesema, ‘Tazama! Nimewaangamiza Waedomu.’+ Kwa hiyo moyo wako umekuwa na kiburi, unataka utukuzwe. Lakini sasa kaa katika nyumba yako mwenyewe.* Kwa nini utafute msiba kisha uanguke, na kuwaangusha pia watu wa Yuda?”

20 Lakini Amazia hakusikiliza,+ kwa sababu Mungu wa kweli alikusudia kuwatia mikononi mwa adui,+ kwa sababu walikuwa wameifuata miungu ya Edomu.+ 21 Basi Mfalme Yehoashi wa Israeli akapanda kwenda huko, naye akapambana vitani na Mfalme Amazia wa Yuda huko Beth-shemeshi,+ jiji la Yuda. 22 Watu wa Yuda wakashindwa na Waisraeli, kwa hiyo kila mmoja akakimbilia nyumbani kwake.* 23 Mfalme Yehoashi wa Israeli akamkamata Mfalme Amazia wa Yuda, mwana wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi,* huko Beth-shemeshi. Kisha akamleta Yerusalemu, naye akabomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu+ mpaka Lango la Pembeni,+ urefu wa mikono 400.* 24 Akachukua dhahabu yote na fedha na vitu vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Mungu wa kweli chini ya Obed-edomu na katika hazina za nyumba ya* mfalme,+ na pia akachukua mateka. Kisha akarudi Samaria.

25 Amazia+ mwana wa Yehoashi mfalme wa Yuda aliendelea kuishi kwa miaka 15 baada ya kifo cha Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.+ 26 Na mambo mengine katika historia ya Amazia, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, je, hayajaandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Yuda na wa Israeli? 27 Kuanzia wakati ambapo Amazia aligeuka na kuacha kumfuata Yehova, walipanga njama+ dhidi yake huko Yerusalemu, akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatie huko Lakishi, nao wakamuua huko. 28 Kwa hiyo wakambeba juu ya farasi na kumrudisha, wakamzika pamoja na mababu zake katika jiji la Yuda.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki