Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 14
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

1 Wafalme—Yaliyomo

      • Unabii wa Ahiya dhidi ya Yeroboamu (1-20)

      • Rehoboamu atawala Yuda (21-31)

        • Shishaki ashambulia (25, 26)

1 Wafalme 14:2

Marejeo

  • +1Fa 11:30, 31

1 Wafalme 14:4

Marejeo

  • +Yos 18:1; 1Sa 4:3

1 Wafalme 14:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Utamwambia hivi na hivi.”

1 Wafalme 14:7

Marejeo

  • +1Fa 11:30, 31; 12:20

1 Wafalme 14:8

Marejeo

  • +1Fa 12:16
  • +1Fa 15:5; Mdo 13:22

1 Wafalme 14:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “sanamu za kuyeyushwa.”

Marejeo

  • +Kum 27:15; 2Nya 11:15
  • +Ne 9:26; Zb 50:17

1 Wafalme 14:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mtu yeyote anayekojoa ukutani.” Huu ni msemo wa Kiebrania wa kuwadharau wanaume.

Marejeo

  • +1Fa 15:25-29

1 Wafalme 14:13

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mkaribie Yehova, uku. 244

    Mnara wa Mlinzi (2010),

    7/1/2010, uku. 29

    7/1/2005, uku. 31

    4/1/1995, uku. 12

  • Fahirishi ya Machapisho

    w10 7/1 29; w05 7/1 31; cl 244

1 Wafalme 14:14

Marejeo

  • +1Fa 15:25-29

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Unabii wa Isaya 1, kur. 133-134

  • Fahirishi ya Machapisho

    ip-1 133-134

1 Wafalme 14:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Kum 8:7-9; 29:28; Yos 23:15; 2Fa 17:6
  • +Kum 28:64; 2Fa 15:29; 18:11
  • +Kum 12:3

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Unabii wa Isaya 1, kur. 133-134

  • Fahirishi ya Machapisho

    ip-1 133-134

1 Wafalme 14:16

Marejeo

  • +1Fa 12:28-30; 13:33, 34

1 Wafalme 14:19

Marejeo

  • +2Nya 12:15; 13:3

1 Wafalme 14:20

Marejeo

  • +2Nya 13:20
  • +1Fa 15:25

1 Wafalme 14:21

Marejeo

  • +Zb 78:68; 132:13
  • +Kut 20:24; Kum 12:5, 6; 1Fa 8:16, 17
  • +1Fa 11:1; 2Nya 12:13

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    12/15/2011, uku. 10

  • Fahirishi ya Machapisho

    w11 12/15 10

1 Wafalme 14:22

Marejeo

  • +1Fa 11:7; 2Nya 12:1
  • +Isa 65:2

1 Wafalme 14:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Kamusi.

Marejeo

  • +Law 26:1
  • +Isa 65:7
  • +Kum 12:2, 3; Isa 57:5; Yer 2:20; Ho. 4:13

1 Wafalme 14:24

Marejeo

  • +Kum 23:17, 18; 1Fa 15:11, 12; 22:46; 2Fa 23:7; Ho. 4:14

1 Wafalme 14:25

Marejeo

  • +1Fa 11:40
  • +2Nya 12:2-4

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    “Kila Andiko,” uku. 295

1 Wafalme 14:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “jumba la mfalme.”

Marejeo

  • +1Fa 7:51; 15:18; 2Fa 18:14, 15; 24:12, 13
  • +1Fa 10:16, 17; 2Nya 12:9-11

1 Wafalme 14:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wakimbiaji.”

1 Wafalme 14:29

Marejeo

  • +1Nya 27:24; 2Nya 12:15

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    3/15/2009, uku. 32

  • Fahirishi ya Machapisho

    w09 3/15 32

1 Wafalme 14:30

Marejeo

  • +1Fa 15:6

1 Wafalme 14:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Anaitwa pia Abiya.

Marejeo

  • +1Fa 11:43
  • +1Fa 11:1; 2Nya 12:13
  • +1Nya 3:10; Mt 1:7

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

1 Fal. 14:21Fa 11:30, 31
1 Fal. 14:4Yos 18:1; 1Sa 4:3
1 Fal. 14:71Fa 11:30, 31; 12:20
1 Fal. 14:81Fa 12:16
1 Fal. 14:81Fa 15:5; Mdo 13:22
1 Fal. 14:9Kum 27:15; 2Nya 11:15
1 Fal. 14:9Ne 9:26; Zb 50:17
1 Fal. 14:101Fa 15:25-29
1 Fal. 14:141Fa 15:25-29
1 Fal. 14:15Kum 8:7-9; 29:28; Yos 23:15; 2Fa 17:6
1 Fal. 14:15Kum 28:64; 2Fa 15:29; 18:11
1 Fal. 14:15Kum 12:3
1 Fal. 14:161Fa 12:28-30; 13:33, 34
1 Fal. 14:192Nya 12:15; 13:3
1 Fal. 14:202Nya 13:20
1 Fal. 14:201Fa 15:25
1 Fal. 14:21Zb 78:68; 132:13
1 Fal. 14:21Kut 20:24; Kum 12:5, 6; 1Fa 8:16, 17
1 Fal. 14:211Fa 11:1; 2Nya 12:13
1 Fal. 14:221Fa 11:7; 2Nya 12:1
1 Fal. 14:22Isa 65:2
1 Fal. 14:23Law 26:1
1 Fal. 14:23Isa 65:7
1 Fal. 14:23Kum 12:2, 3; Isa 57:5; Yer 2:20; Ho. 4:13
1 Fal. 14:24Kum 23:17, 18; 1Fa 15:11, 12; 22:46; 2Fa 23:7; Ho. 4:14
1 Fal. 14:251Fa 11:40
1 Fal. 14:252Nya 12:2-4
1 Fal. 14:261Fa 7:51; 15:18; 2Fa 18:14, 15; 24:12, 13
1 Fal. 14:261Fa 10:16, 17; 2Nya 12:9-11
1 Fal. 14:291Nya 27:24; 2Nya 12:15
1 Fal. 14:301Fa 15:6
1 Fal. 14:311Fa 11:43
1 Fal. 14:311Fa 11:1; 2Nya 12:13
1 Fal. 14:311Nya 3:10; Mt 1:7
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
1 Wafalme 14:1-31

Kitabu cha Kwanza cha Wafalme

14 Wakati huo Abiya mwana wa Yeroboamu akawa mgonjwa. 2 Kwa hiyo Yeroboamu akamwambia mke wake: “Tafadhali, inuka, badili sura yako ili watu wasitambue kwamba wewe ni mke wa Yeroboamu, halafu uende Shilo. Tazama! Nabii Ahiya yuko huko. Yeye ndiye aliyesema kwamba mimi nitakuwa mfalme wa watu hawa.+ 3 Chukua mikate kumi, keki zilizonyunyiziwa kitu, na chupa ya asali, uende kwake. Kisha atakwambia kitakachompata mvulana huyu.”

4 Mke wa Yeroboamu akafanya mambo aliyoambiwa na Yeroboamu. Akainuka na kwenda Shilo,+ akafika katika nyumba ya Ahiya. Ahiya alikodoa macho yake mbele, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umri wake.

5 Hata hivyo, Yehova alikuwa amemwambia Ahiya: “Tazama, mke wa Yeroboamu anakuja kutafuta habari kuhusu mwanawe, kwa sababu ni mgonjwa. Nitakwambia mambo utakayomwambia.* Atakapofika ataficha sura yake ili asijulikane.”

6 Mara tu Ahiya aliposikia sauti ya miguu ya mwanamke huyo alipokuwa akija mlangoni, akasema: “Ingia ndani, mke wa Yeroboamu. Kwa nini unaficha sura yako usijulikane? Nimeagizwa nikupe ujumbe mkali. 7 Nenda, ukamwambie Yeroboamu, ‘Hivi ndivyo anavyosema Yehova Mungu wa Israeli: “Nilikuinua kutoka miongoni mwa watu wako na kukufanya kuwa kiongozi wa watu wangu Waisraeli.+ 8 Kisha nikaurarua ufalme kutoka katika nyumba ya Daudi na kukupa wewe.+ Lakini hujawa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye alishika amri zangu na kunifuata kwa moyo wake wote, akitenda tu yaliyokuwa sawa machoni pangu.+ 9 Lakini umetenda mambo mabaya zaidi kuliko wote waliokutangulia, nawe ulijitengenezea mungu mwingine na sanamu za chuma* ili kunikasirisha,+ mimi ndiye uliyenigeuzia mgongo.+ 10 Kwa sababu hiyo ninailetea msiba nyumba ya Yeroboamu, nami nitamwangamiza kila mwanamume* wa Yeroboamu, kutia ndani wasio na uwezo na walio dhaifu katika Israeli, nami nitaifagia kabisa nyumba ya Yeroboamu,+ kama mtu anavyoondoa kabisa mavi mpaka yote yanapokwisha! 11 Mtu yeyote wa Yeroboamu atakayefia jijini, ataliwa na mbwa; na yeyote atakayefia shambani, ataliwa na ndege wa angani, kwa sababu Yehova amesema hayo.”’

12 “Sasa inuka; nenda nyumbani kwako. Utakapotia mguu wako jijini, mtoto huyo atakufa. 13 Waisraeli wote watamwombolezea na kumzika, kwa maana ni yeye peke yake katika familia ya Yeroboamu atakayezikwa kaburini, kwa sababu ni yeye tu katika nyumba ya Yeroboamu ambaye Yehova Mungu wa Israeli amepata jambo fulani jema ndani yake. 14 Yehova atajiinulia mfalme wa Israeli atakayeiangamiza nyumba ya Yeroboamu+ kuanzia siku hiyo na kuendelea, naam, hata sasa. 15 Yehova atawapiga Waisraeli kama tete linaloyumba-yumba ndani ya maji, naye atawang’oa Waisraeli kutoka katika nchi hii nzuri aliyowapa mababu zao+ na kuwatawanya ng’ambo ya Mto Efrati,+ kwa sababu walimkasirisha Yehova kwa kutengeneza miti mitakatifu.*+ 16 Naye atawaacha Waisraeli kwa sababu ya dhambi ambazo Yeroboamu alitenda na kusababisha Waisraeli kuzitenda.”+

17 Basi mke wa Yeroboamu akainuka na kwenda zake, akafika Tirsa. Alipokaribia kizingiti cha mlango, mvulana huyo akafa. 18 Kwa hiyo wakamzika, na Waisraeli wote wakamwombolezea, kama Yehova alivyokuwa amesema kupitia nabii Ahiya, mtumishi wake.

19 Na mambo mengine katika historia ya Yeroboamu, jinsi alivyopigana vita+ na jinsi alivyotawala, yameandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli. 20 Yeroboamu alitawala kwa miaka 22, kisha akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake;+ na Nadabu mwanawe akawa mfalme baada yake.+

21 Wakati huo, Rehoboamu mwana wa Sulemani alikuwa mfalme wa Yuda. Rehoboamu alikuwa na umri wa miaka 41 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 17 huko Yerusalemu, jiji ambalo Yehova alichagua+ miongoni mwa makabila yote ya Israeli ili kuweka jina lake humo.+ Mama ya Rehoboamu aliitwa Naama, naye alikuwa Mwamoni.+ 22 Na watu wa Yuda walikuwa wakitenda maovu machoni pa Yehova,+ na kwa dhambi zao walimkasirisha kuliko walivyofanya mababu zao.+ 23 Pia waliendelea kujijengea mahali pa juu, nguzo takatifu, na miti mitakatifu*+ juu ya kila kilima kirefu+ na chini ya kila mti wenye majani mengi.+ 24 Kulikuwa pia na wanaume makahaba wa hekaluni katika nchi.+ Watu walitenda mambo yote yenye kuchukiza yaliyofanywa na mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli.

25 Katika mwaka wa tano wa Mfalme Rehoboamu, Mfalme Shishaki+ wa Misri alishambulia Yerusalemu.+ 26 Akachukua hazina za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya mfalme.*+ Alichukua kila kitu, kutia ndani ngao zote za dhahabu ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza.+ 27 Basi Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba zichukue mahali pa ngao hizo, akaziweka chini ya ulinzi wa mkuu wa walinzi,* aliyelinda mlango wa nyumba ya mfalme. 28 Wakati wowote ambapo mfalme alikuja katika nyumba ya Yehova, walinzi walizichukua, kisha walizirudisha katika chumba cha walinzi.

29 Na mambo mengine katika historia ya Rehoboamu, mambo yote aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda?+ 30 Kulikuwa na vita daima kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.+ 31 Kisha Rehoboamu akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi.+ Mama yake aliitwa Naama, naye alikuwa Mwamoni.+ Na Abiyamu* mwana wake+ akawa mfalme baada yake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki