NAHUMU
1 Tangazo dhidi ya Ninawi:+ Kitabu cha maono ya Nahumu* Mwelkoshi:
2 Yehova ni Mungu anayetaka watu wamwabudu yeye peke yake+ naye hulipiza kisasi;
Yehova hulipiza kisasi naye yuko tayari kuonyesha ghadhabu yake.+
Yehova hulipiza kisasi dhidi ya maadui wake,
Naye hukusanya ghadhabu kwa ajili ya maadui wake.
3 Yehova si mwepesi wa hasira,+ naye ana nguvu nyingi,+
Lakini Yehova hatasita kamwe kutoa adhabu inayostahiliwa.+
Kijia chake kimo katika upepo unaosababisha uharibifu na katika dhoruba,
Na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.+
Bashani na Karmeli hunyauka,+
Na maua ya Lebanoni hunyauka.
Dunia itasukasuka kwa sababu ya uso wake,
Pamoja na nchi na wote wanaoishi humo.+
6 Ni nani anayeweza kusimama mbele ya hasira yake kali?+
Na ni nani anayeweza kustahimili joto la hasira yake?+
Ghadhabu yake itamwagwa kama moto,
Na miamba itavunjika-vunjika kwa sababu yake.
7 Yehova ni mwema,+ ni ngome katika siku ya taabu.+
Anawakazia fikira* wale wanaotafuta kimbilio kwake.+
9 Mtapanga njama gani dhidi ya Yehova?
Anasababisha maangamizi kamili.
Taabu haitatokea tena mara ya pili.+
10 Kwa maana wamesokotana kama miiba,
Nao ni kama watu waliolewa pombe;*
Lakini watateketezwa kabisa kama nyasi kavu.
11 Kutoka kwako atatoka yule anayepanga njama ya uovu dhidi ya Yehova,
Akitoa ushauri usiofaa.
12 Yehova anasema hivi:
“Ingawa walikuwa na nguvu nyingi na walikuwa wengi,
Hata hivyo, wataangamizwa na kutoweka.*
Nimekutesa wewe,* lakini sitakutesa tena.
Nitaziharibu sanamu zako za kuchongwa na sanamu za chuma* kutoka katika nyumba ya* miungu yako.
Nitakuchimbia kaburi, kwa sababu unachukiza.’
Fanya sherehe zako,+ Ee Yuda, timiza nadhiri zako,
Kwa maana mtu asiyefaa hatapita tena kati yako.
Ataangamizwa kabisa.”
2 Yule anayetawanya amekuvamia.*+
Linda ngome.
Linda njia.
Jitayarisheni* na mkusanye nguvu zenu zote.
2 Kwa maana Yehova atarudisha fahari ya Yakobo,
Pamoja na fahari ya Israeli,
Kwa sababu waangamizaji wamewaangamiza;+
Nao wameharibu machipukizi yao.
3 Ngao za wanaume wake hodari zimetiwa rangi nyekundu,
Mashujaa wake wamevaa nguo nyekundu.
Vyuma vya magari yake ya vita vinawakawaka kama moto
Katika siku anayojitayarisha kwa ajili ya vita,
Na mikuki ya miberoshi inapotikiswa.
4 Magari ya vita yanaendeshwa kwa kasi sana barabarani.
Yanakimbia huku na huku katika viwanja vya mji.
Yanang’aa kama mienge inayowaka na kumweka kama radi.
5 Atawaita maofisa wake.
Watajikwaa wanaposonga mbele.
Wanakimbilia haraka kwenye ukuta wake;
Wanaweka kizuizi.
Amechukuliwa, na vijakazi wake wanalia kwa huzuni;
Wanalia kama njiwa huku wakijipigapiga vifua.*
“Simameni tuli! Simameni tuli!”
Lakini hakuna yeyote anayegeuka nyuma.+
9 Poreni fedha, poreni dhahabu!
Hazina zake haziishi.
Zimejazwa kila aina ya vitu vyenye thamani.
10 Jiji liko tupu, liko ukiwa, na limeharibiwa kabisa!+
Mioyo yao inayeyuka kwa woga, magoti yao yanalegea, viuno vyao vinatetemeka;
Nyuso zao zote zimebadilika rangi.
11 Liko wapi pango la simba,+ mahali ambapo wanasimba* wanakula,
Mahali ambapo simba anatoka akimwongoza mtoto wake,
Na hakuna yeyote wa kuwaogopesha?
12 Simba aliwararulia watoto wake mawindo ya kutosha,
Akayakaba pumzi mawindo kwa ajili ya majike yake.
Alijaza mawindo katika mapango yake,
Makao yake akayajaza wanyama walioraruliwa.
13 “Tazama! Niko dhidi yako,” asema Yehova wa majeshi,+
“Nitayateketeza kwa moto magari yake ya vita,+
Na upanga utawachinja wanasimba wako.*
Nitayaangamiza kabisa mawindo yako duniani,
Na sauti ya wajumbe wako haitasikika tena.”+
3 Ole kwa jiji la umwagaji wa damu!
Limejaa kabisa udanganyifu na unyang’anyi.
Halikosi kamwe mawindo!
2 Kuna sauti ya mjeledi na mlio wa magurudumu,
Farasi anayekimbia kasi na gari la vita linalorukaruka.
3 Mpanda farasi aliye juu ya farasi, upanga unaomweka, na mkuki unaometameta,
Umati wa watu waliouawa na marundo ya maiti
—Maiti hazihesabiki.
Wanaendelea kujikwaa juu ya maiti.
4 Yote hayo ni kwa sababu ya matendo mengi ya ukahaba yaliyotendwa na huyo kahaba,
Aliye mrembo na mwenye kuvutia, bimkubwa wa uchawi,
Anayeyanasa mataifa kwa ukahaba wake na familia kwa uchawi wake.
5 “Tazama! Niko dhidi yako,”* asema Yehova wa majeshi,+
“Nitainua nguo yako juu na kufunika uso wako;
Nitayafanya mataifa yaone uchi wako,
Na falme zione aibu yako.
Ni nani atakayelihurumia?’
Nitakutafutia wapi wafariji?
8 Je, wewe ni bora kuliko jiji la No-amoni,*+ lililoketi kando ya mifereji ya Nile?+
Maji yalilizunguka;
Utajiri wake ulikuwa bahari na ukuta wake ulikuwa bahari.
9 Nchi ya Ethiopia ilikuwa chanzo cha nguvu zake zisizo na mipaka, pia Misri.
Putu+ na Walibya walikusaidia.+
Watoto wake pia walipondwa-pondwa katika kila pembe ya barabara.
Walipiga kura ili kuwauza wanaume wake wanaoheshimiwa,
Na wanaume wake wote wakuu wamefungwa kwa pingu.
Utatafuta kimbilio kutoka kwa adui.
12 Ngome zako zote ni kama mitini yenye tini za kwanza zilizoiva;
Zikitikiswa, zitaanguka kinywani mwa walaji walafi.
13 Tazama! Wanajeshi wako ni kama wanawake kati yako.
Malango ya nchi yako yatakuwa wazi kabisa kwa ajili ya maadui wako.
Moto utateketeza kabisa makomeo ya malango yako.
14 Teka maji kabla hujazingirwa!+
Imarisha ngome zako.
Shuka chini kwenye matope na kukanyagakanyaga udongo wa mfinyanzi;
Chukua chombo cha kufyatulia matofali.
15 Hata huko moto utakuteketeza kabisa.
Upanga utakukatakata.+
Utakutafuna kama nzige wachanga wanavyofanya.+
Ongezeka sana kama nzige wachanga!
Naam, ongezeka sana kama nzige!
16 Umezidisha wafanyabiashara wako kuliko nyota za mbinguni.
Nzige mchanga hujivua ngozi kisha huruka na kwenda zake.
17 Walinzi wako ni kama nzige,
Na maofisa wako ni kama kundi la nzige.
Wanapiga kambi katika mazizi ya mawe siku yenye baridi,
Lakini jua linapowaka, wao huruka na kwenda zao;
Na hakuna yeyote anayejua mahali walipo.
18 Wachungaji wako wanasinzia, Ee mfalme wa Ashuru;
Wakuu wako wanakaa katika makao yao.
Watu wako wametawanyika milimani,
Na hakuna yeyote anayewakusanya pamoja.+
19 Msiba wako hauna kitulizo.
Jeraha lako haliwezi kuponywa.
Wale wote wanaosikia habari zako watapiga makofi;+
Kwa maana ni nani ambaye hajateseka kwa sababu ya ukatili wako usio na mwisho?”+
Maana yake “Mfariji.”
Au “Anawatunza.” Tnn., “Anawajua.”
Yaani, Ninawi.
Au “pombe ya ngano.”
Au labda, “naye atapita katikati yake.”
Yaani, watu wa Yuda.
Yaani, Ashuru.
Au “sanamu za kuyeyushwa.”
Au “hekalu la.”
Yaani, Ninawi.
Tnn., “Imarisheni viuno.”
Au “litaporomoka.”
Au “Imeagizwa.”
Tnn., “mioyo.”
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Au “wanasimba wako wenye manyoya marefu shingoni.”
Yaani, Ninawi.
Au “kitu cha kuchekesha.”
Yaani, Thebesi.