Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Agosti 9
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme. Kama madokezo kwenye ukurasa wa 8 yanafaa eneo la kutaniko lenu, yatumie kuonyesha jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi, Julai 15 na Amkeni!, Julai 22. Utoaji mwingine unaweza kutumiwa. Eleza kuhusu mpango wa michango. Wakumbushe wasikilizaji wabebe broshua Anataka juma lijalo.
Dak. 15: “Uvumilivu Unathawabishwa.”a Tia ndani maelezo machache kutoka Mnara wa Mlinzi, Desemba 15, 2000, ukurasa wa 22-23, fungu la 15-18.
Dak. 20: Kutumia Trakti ili Kuanzisha Mafunzo ya Biblia. Hotuba pamoja na mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 2002, ukurasa wa 3-4. Kazia kwamba tuko tayari kubadilika kulingana na hali za kila mwanafunzi, kama inavyoonyeshwa katika fungu la 5. Tia ndani onyesho moja au mawili mafupi yanayotegemea fungu la 8-10. Ikiwa utoaji mwingine una matokeo kwenu, eleza na utoe onyesho la utoaji huo badala yake. Waombe wasikilizaji wasimulie mambo waliyoona wakitumia trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia?
Wimbo 74 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 16
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Kaza Kweli Kikiki Katika Mtoto Wako. Hotuba ikitegemea kitabu Furaha ya Familia, ukurasa wa 55-59. Zungumzia zile njia nne ambazo wazazi wanaweza kutumia kuwasaidia watoto wao wasitawishe uhusiano wa karibu na wa kibinafsi pamoja na Yehova, na kuonyesha jinsi habari hizo zinavyotumika.
Dak. 20: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo—Sehemu ya 2.”b Tia ndani onyesho la dakika tano. Mhubiri amuuliza mzee jinsi ya kumsaidia mwanafunzi wa Biblia kufanya maendeleo. Mzee anataja kwamba mara nyingi wahubiri huanguka katika mtego wa kutumia muda mwingi mno wakati wa funzo kuzungumzia mambo madogo na yale yasiyo ya lazima. Akitumia somo la 9 la broshua Anataka, anamwonyesha mhubiri jinsi ya (1) kukazia mambo makuu katika habari, (2) kutumia kwa matokeo maandiko yaliyoonyeshwa bila kunukuliwa, na (3) kufanya somo hilo lifae mahitaji ya mwanafunzi. Anataja kwamba matayarisho mazuri yanahitajika kila mara funzo linapoongozwa.
Wimbo 85 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 23
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Toa onyesho la jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi, Agosti 1 na Amkeni!, Agosti 8. Katika utoaji mmoja, onyesha mhubiri akimtolea mwalimu wa shule ushahidi.
Dak. 10: “Mpango Mpya wa Kupitia Programu za Makusanyiko.” Hotuba pamoja na mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea makala kwenye ukurasa wa 4. Taja tarehe za kusanyiko lijalo la mzunguko na la pekee ikiwa zinapatikana. Wale wanaotaka kubatizwa wanapaswa kumjulisha mapema mwangalizi-msimamizi.
Dak. 20: Kutoa Kitabu Muumba Mwezi wa Septemba. Hotuba na onyesho. Taja baadhi ya maelezo ambayo yametolewa kuhusu kichapo hicho. (w99 6/15 uku. 25-26) Toa muhtasari wa yaliyomo katika kitabu, na kazia mambo fulani hususa ambayo yanaweza kuwavutia watu katika eneo lenu. (km 2/99 uku. 2; km 4/99 uku. 2; km 9/99 uku. 2) Taja utoaji rahisi unaotia ndani utangulizi fulani kutoka katika kitabu Kutoa Sababu au Huduma Yetu ya Ufalme, andiko, na jambo au sura fulani katika kitabu Muumba. Mhubiri mwenye uwezo atoe onyesho hilo. Ikiwa kitabu Muumba hakipatikani, badili utoaji huo ufae toleo la badala.
Wimbo 220 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 30
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Agosti.
Dak. 15: “Shule ya Mazoezi ya Kihuduma—Mlango Mkubwa Unaoongoza Kwenye Utendaji.” Hotuba pamoja na mazungumzo na wasikilizaji. Tia ndani maelezo kutoka katika Kitabu cha Mwaka cha 2004, ukurasa wa 239-240. Taja mkutano kwa ajili ya wale wanaopendezwa kuhudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma, ambao hufanywa kwenye kusanyiko la mzunguko. Watie moyo wale wanaostahili wahudhurie mkutano huo.
Dak. 20: Je, Umefaidika? Mazungumzo na wasikilizaji. Pitia madokezo yafuatayo yaliyokuwa katika Huduma Yetu ya Ufalme katika mwaka uliopita wa utumishi: Andika utangulizi wako kwenye karatasi ndogo. (km 10/03 uku. 8) Mpongeze mtu binafsi, kihususa na kutoka moyoni. (km 11/03 uku. 1) Hubiri wakati ambapo kuna uwezekano mkubwa wa kuwapata watu nyumbani. (km 12/03 uku. 1) Tenga wakati hususa kwa ajili ya kusoma Biblia, kutayarisha mikutano, na kuhubiri shambani. (km 1/04 uku. 4) Tumia broshua “Nchi Nzuri” unapofanya funzo la kibinafsi na usomaji wa Biblia. (km 3/04 uku. 2) Weka mradi wa kusoma Biblia nzima. (km 4/04 uku. 1) Hubiri katika eneo la biashara. (km 7/04 uku. 4) Tumia trakti kuanzisha mafunzo ya Biblia. (km 8/04 uku. 2) Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu faida walizopokea kwa kutumia madokezo hayo.
Wimbo 145 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 6
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 25: “Onyesha Roho ya Upainia.”c Mhoji kwa kifupi painia mmoja au wawili. Waombe watoe maelezo kuhusu jinsi kielelezo cha wazazi, wazee, au wengine kilivyowatia moyo wafuatie huduma ya wakati wote.
Wimbo 142 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.