Zaburi
3 Uwe kwangu ngome ya mwamba ya kuingia ndani daima.+
Utoe amri ili kuniokoa,+
Kwa maana wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.+
4 Ee Mungu wangu, uniokoe na mkono wa mwovu,+
Na mkono wa mtu anayetenda kwa njia isiyo ya haki na kwa ukandamizaji.+
5 Kwa maana wewe ni tumaini langu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova, tegemeo langu tangu ujana wangu.+
6 Nimekutegemea tangu tumboni;+
Wewe ndiye Yule anayenitenganisha na sehemu za ndani za mama yangu.+
Sifa yangu kwako ni ya daima.+
10 Kwa maana adui zangu wamesema juu yangu,+
Na walewale wanaoitafuta nafsi yangu wameshauriana pamoja,+
13 Hao na waaibike, hao na wafikie mwisho wao, wanaoshindana na nafsi yangu.+
Hao na wajifunike kwa shutuma na fedheha wanaonitafutia msiba.+
15 Kinywa changu mwenyewe kitasimulia uadilifu wako,+
Wokovu wako mchana kutwa,+
Kwa maana sijapata kujua hesabu yake.+
16 Nitaingia na nguvu kuu,+ Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu+ Yehova;
Nitautangaza uadilifu wako, naam, wako peke yako.+
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu,+
Na mpaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako za ajabu.+
18 Na mpaka wakati wa uzee na wa kuwa na kichwa chenye mvi, Ee Mungu, usiniache,+
Mpaka nikitangazie kizazi habari za mkono wako,+
Habari za nguvu zako, kwa wale wote watakaokuja.+
19 Uadilifu wako, Ee Mungu, unafika kileleni;+
Na kuhusu mambo makuu ambayo umeyafanya,+
Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?+
20 Kwa sababu umenifanya nione taabu nyingi na misiba,+
Unifufue tena;+
Na unipandishe tena kutoka katika vilindi vya maji vya dunia.+
22 Mimi pia, nitakusifu kwa chombo cha kinanda,+
Kuhusu ukweli wako, Ee Mungu wangu.+
Nitakupigia muziki kwa kinubi, Ee Mtakatifu wa Israeli.+