Zaburi
Maskili. Ya Asafu.+
74 Kwa nini, Ee Mungu, umetutupilia mbali milele?+
Kwa nini hasira yako inatoa moshi daima juu ya kundi la malisho yako?+
2 Ulikumbuke kusanyiko lako ulilojipatia zamani za kale,+
Kabila ulilolikomboa liwe urithi wako,+
Huu Mlima Sayuni ambapo umekaa.+
3 Uziinue hatua zako kwenye ukiwa wenye kudumu muda mrefu.+
Kila kitu katika mahali patakatifu adui amekitendea vibaya.+
4 Wale wanaokuonyesha uadui wamenguruma katikati ya mahali pa kukutania.+
Wameweka ishara zao wenyewe kuwa ndizo ishara.+
5 Mtu ana sifa mbaya ya kuwa kama yule anayeinua mashoka juu ya kichaka cha miti.
6 Na sasa vitu vyake vilivyochongwa, kila kimoja, wao wanakipiga hata kwa kishoka na kwa mipini yenye ncha za chuma.+
8 Wao, hata uzao wao, wamesema pamoja moyoni mwao:
“Mahali pote pa kukutania pa Mungu katika nchi lazima pateketezwe.”+
10 Ee Mungu, mpinzani ataendelea kushutumu mpaka wakati gani?+
Je, adui ataendelea kulidharau jina lako milele?+
11 Kwa nini unaendelea kuuondoa mkono wako, naam, mkono wako wa kuume+
Kutoka katikati ya kifua chako ili kutumaliza sisi?
12 Hata hivyo Mungu ni Mfalme wangu tangu zamani za kale,+
Yeye anayefanya wokovu mkuu katikati ya dunia.+
13 Wewe mwenyewe uliichochea bahari kwa nguvu zako mwenyewe;+
Ulivunja vichwa vya wanyama wakubwa wa baharini katika maji.+
14 Wewe mwenyewe uliponda vipande-vipande vichwa vya Lewiathani.*+
Ukawapa watu kuwa chakula, wale wanaokaa katika maeneo yasiyo na maji.+
17 Ni wewe uliyeweka mipaka yote ya dunia;+
Majira ya kiangazi na majira ya baridi kali—wewe mwenyewe uliyafanyiza.+
18 Ukumbuke hili: Adui ameshutumu, Ee Yehova,+
Na kikundi cha watu wasio na akili kimelidharau jina lako.+
21 Mtu aliyepondwa na asirudi akiwa amefedheheshwa.+
Mwenye kuteseka na maskini na walisifu jina lako.+