Zaburi
Kwa kiongozi wa Muth-labeni. Muziki wa Daudi.
א [ʼAʹleph]
ב [Behth]
4 Kwa maana umetekeleza hukumu yangu na kesi yangu;+
Umeketi juu ya kiti cha ufalme ukihukumu kwa uadilifu.+
ג [Giʹmel]
5 Umeyakemea mataifa,+ umemwangamiza mwovu.+
Jina lao umelifutilia mbali mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
6 Ewe adui, ukiwa wako umefikia mwisho wake wa kudumu,+
Na majiji ambayo umeyang’oa.+
Kumbukumbu lao hakika litaangamia.+
ה [Heʼ]
7 Yeye Yehova ataketi mpaka wakati usio na kipimo,+
Akifanya imara kiti chake cha ufalme kwa ajili ya hukumu.+
8 Naye mwenyewe ataihukumu kwa uadilifu nchi yenye kuzaa;+
Atavihukumu vikundi vya mataifa kwa unyoofu.+
ו [Waw]
9 Naye Yehova atakuwa kilele salama kwa ajili ya mtu yeyote aliyekandamizwa,+
Kilele salama wakati wa taabu.+
10 Na wale wanaolijua jina lako watakutegemea,+
Kwa maana hakika hutawaacha wale wanaokutafuta, Ee Yehova.+
ז [Zaʹyin]
11 Mpigieni Yehova muziki, yeye anayekaa Sayuni;+
Tangazeni matendo yake katikati ya vikundi vya watu.+
12 Kwa maana, wakati wa kutafuta umwagikaji wa damu,+ hakika atawakumbuka hao;+
Hakika yeye hatakisahau kilio cha wenye kuteseka.+
ח [Chehth]
13 Unionyeshe kibali, Ee Yehova; uone mateso yangu kutoka kwa wale wanaonichukia,+
Ewe unayeniinua kutoka katika malango ya kifo,+
14 Ili niyatangaze matendo yako yote yanayostahili sifa+
Katika malango+ ya binti Sayuni,+
Ili niushangilie wokovu wako.+
ט [Tehth]
16 Yehova anajulikana kwa hukumu ambayo ametekeleza.+
Mwovu amenaswa na utendaji wa mikono yake mwenyewe.+
Higayoni. Sela.
י [Yohdh]
כ [Kaph]