Zekaria
2 Nami nikainua macho yangu nikaona; na tazama! kulikuwa na mtu, naye alikuwa na kamba ya kupimia+ mkononi mwake. 2 Basi nikasema: “Unaenda wapi?”
Naye akaniambia: “Kupima Yerusalemu, ili kuona jinsi upana wake ulivyo na jinsi urefu wake ulivyo.”+
3 Na tazama! malaika aliyekuwa akisema nami akatoka, na kulikuwa na malaika mwingine akitoka kwenda kukutana naye. 4 Ndipo akamwambia: “Kimbia, useme na yule kijana pale, umwambie, “ ‘Yerusalemu litakaliwa na watu+ kama nchi ya mashambani iliyo wazi, kwa sababu ya wingi wa watu na wanyama wa kufugwa walio ndani yake.+ 5 Nami mwenyewe nitakuwa kwake,” asema Yehova, “ukuta wa moto kuzunguka pande zote,+ nami nitakuwa utukufu ndani yake.” ’ ”+
6 “Haya! Haya! Ikimbieni basi, nchi ya kaskazini,”+ asema Yehova.
“Maana nimewatawanya ninyi kotekote kuelekea pepo nne za mbingu,”+ asema Yehova.
7 “Haya, Sayuni!+ Ponyoka, wewe unayekaa na binti Babiloni.+ 8 Kwa maana Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Baada ya utukufu+ amenituma kwa mataifa yaliyokuwa yakiwapora ninyi;+ kwa maana yeye anayewagusa ninyi+ anaigusa mboni ya jicho langu.+ 9 Maana tazama, ninatikisa mkono wangu juu yao,+ nao watakuwa nyara kwa watumwa wao.’+ Nanyi mtajua ya kwamba Yehova wa majeshi amenituma mimi.+
10 “Paaza sauti na kushangilia, Ee binti Sayuni;+ kwa maana mimi naja,+ nami nitakaa katikati yako,”+ asema Yehova. 11 “Na mataifa mengi yatajiunga na Yehova siku hiyo,+ nao watakuwa watu wangu;+ nami nitakaa katikati yako.” Nawe utajua kwamba Yehova wa majeshi amenituma kwako.+ 12 Na Yehova atamiliki Yuda iwe fungu lake katika nchi takatifu,+ naye atalichagua Yerusalemu tena.+ 13 Nyamazeni, watu wote, mbele za Yehova,+ kwa maana ameamka+ kutoka katika makao yake matakatifu.+