Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 41:52
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 52 Naye yule wa pili akamwita jina lake Efraimu,+ kwa sababu, kama alivyosema, “Mungu ameniwezesha kuwa na uzao katika nchi ya taabu yangu.”+

  • Mwanzo 46:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Na katika nchi ya Misri Yosefu alizaa, Manase+ na Efraimu,+ ambao Asenathi+ binti ya Potifera kuhani wa Oni alimzalia.

  • Mwanzo 48:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Lakini baba yake akaendelea kukataa, akisema: “Najua, mwanangu, najua. Yeye pia atakuwa kikundi cha watu naye pia atakuwa mkuu.+ Lakini, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye,+ nao uzao wake utakuwa hesabu kamili ya mataifa.”+

  • Hesabu 2:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya Efraimu+ kwa majeshi yao utakuwa kuelekea magharibi, na mkuu wa wana wa Efraimu ni Elishama+ mwana wa Amihudi.

  • Hesabu 26:35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Hawa ndio waliokuwa wana wa Efraimu+ kulingana na familia zao: Wa Shuthela+ familia ya Washuthela; wa Bekeri familia ya Wabekeri; wa Tahani+ familia ya Watahani.

  • Kumbukumbu la Torati 33:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kama mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe-dume ndivyo fahari yake ilivyo,+

      Na pembe zake ni pembe za ng’ombe-dume wa mwituni.+

      Atasukuma vikundi vya watu kwa pembe hizo+

      Wote pamoja mpaka miisho ya dunia,

      Nao ni makumi ya maelfu ya Efraimu,+

      Nao ni maelfu ya Manase.”

  • Waamuzi 12:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 ndipo walipomwambia: “Tafadhali sema Shibolethi.”+ Naye alisema: “Sibolethi,” kwa kuwa hakuweza kutamka neno hilo kwa usahihi. Nao walimshika na kumuua kwenye vivuko vya Yordani. Basi wakati huo wakaanguka watu 42,000 kutoka katika Efraimu.+

  • Yeremia 7:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Nami nitawatupa ninyi nje kutoka mbele za macho yangu,+ kama nilivyowatupa nje ndugu zenu wote, uzao wote wa Efraimu.’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki