Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 28:63
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 63 “Na itatukia kwamba kama vile Yehova alivyokuwa na furaha juu yenu ili kuwafanyia mema na kuwazidisha ninyi,+ ndivyo Yehova atakavyokuwa na furaha juu yenu ili kuwaharibu ninyi na kuwaangamiza ninyi;+ nanyi mtang’olewa kutoka katika nchi mnayoenda kuimiliki.+

  • 1 Wafalme 14:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Na kwa kweli Yehova atawapiga Israeli, kama vile tu tete linavyoyumba-yumba majini;+ naye atawang’oa+ Israeli kutoka katika nchi hii nzuri+ aliyowapa mababu zao, naye atawatawanya+ ng’ambo ya ule Mto,+ kwa sababu walitengeneza miti yao mitakatifu,+ na hivyo kumtia uchungu+ Yehova.

  • 2 Wafalme 17:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Kwa hiyo Yehova akakasirikia+ Israeli sana, hivi kwamba akawaondoa machoni pake.+ Hakuacha yeyote abaki isipokuwa kabila la Yuda peke yake.+

  • Zaburi 52:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Mungu mwenyewe pia atakubomoa milele;+

      Atakupiga na kukuangusha na kukurarua kutoka katika hema lako,+

      Naye atakung’oa kutoka katika nchi ya walio hai.+ Sela.

  • Luka 21:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 nao wataanguka kwa makali ya upanga na watapelekwa mateka katika mataifa yote;+ na Yerusalemu litakanyagwa-kanyagwa na mataifa, mpaka nyakati zilizowekwa+ za mataifa zitimie.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki