40 Nanyi mtajichukulia katika siku ya kwanza tunda la miti yenye fahari, matawi ya mitende+ na matawi ya miti yenye majani mengi na mierebi ya bonde la mto, nanyi mtashangilia+ mbele za Yehova Mungu wenu siku saba.
12 Nanyi mtashangilia mbele za Yehova Mungu wenu,+ ninyi na wana wenu na binti zenu na watumishi wenu na vijakazi wenu na Mlawi aliye ndani ya malango yenu, kwa sababu hana fungu wala urithi pamoja nanyi.+
18 Lakini mbele za Yehova Mungu wako utaila, katika mahali ambapo Yehova Mungu wako atachagua,+ wewe na mwana wako na binti yako na mtumishi wako na kijakazi wako na Mlawi aliye ndani ya malango yako; nawe utashangilia+ mbele za Yehova Mungu wako katika kazi zako zote.
26 Nawe utatoa pesa hizo kwa ajili ya chochote ambacho nafsi yako itatamani+ kati ya ng’ombe na kondoo na mbuzi na divai na kileo+ na kitu chochote ambacho huenda nafsi yako ikakuomba; nawe utakula huko mbele za Yehova Mungu wako na kushangilia,+ wewe na nyumba yako.