Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 23:40
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 40 Nanyi mtajichukulia katika siku ya kwanza tunda la miti yenye fahari, matawi ya mitende+ na matawi ya miti yenye majani mengi na mierebi ya bonde la mto, nanyi mtashangilia+ mbele za Yehova Mungu wenu siku saba.

  • Kumbukumbu la Torati 12:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Nanyi mtashangilia mbele za Yehova Mungu wenu,+ ninyi na wana wenu na binti zenu na watumishi wenu na vijakazi wenu na Mlawi aliye ndani ya malango yenu, kwa sababu hana fungu wala urithi pamoja nanyi.+

  • Kumbukumbu la Torati 12:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Lakini mbele za Yehova Mungu wako utaila, katika mahali ambapo Yehova Mungu wako atachagua,+ wewe na mwana wako na binti yako na mtumishi wako na kijakazi wako na Mlawi aliye ndani ya malango yako; nawe utashangilia+ mbele za Yehova Mungu wako katika kazi zako zote.

  • Kumbukumbu la Torati 14:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Nawe utatoa pesa hizo kwa ajili ya chochote ambacho nafsi yako itatamani+ kati ya ng’ombe na kondoo na mbuzi na divai na kileo+ na kitu chochote ambacho huenda nafsi yako ikakuomba; nawe utakula huko mbele za Yehova Mungu wako na kushangilia,+ wewe na nyumba yako.

  • Zaburi 32:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Shangilieni katika Yehova na kuwa na shangwe, enyi waadilifu;+

      Na mpige vigelegele vya shangwe, ninyi nyote mlio wanyoofu katika moyo.+

  • Zaburi 100:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Mtumikieni Yehova kwa kushangilia.+

      Njooni mbele zake kwa vigelegele vya shangwe.+

  • Wafilipi 4:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Shangilieni sikuzote katika Bwana.+ Mara nyingine tena nitasema, Shangilieni!+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki