17 Na Samweli akaendelea kusema: “Je, haikuwa wakati ulipokuwa mdogo machoni pako mwenyewe+ kwamba ukawa kichwa cha makabila ya Israeli, na Yehova akakutia mafuta+ uwe mfalme juu ya Israeli?
25 Lakini Hezekia hakurudisha kulingana na mema aliyotendewa,+ kwa kuwa moyo wake ulikuwa wenye majivuno+ na kukawa na ghadhabu+ juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu.
42 Lakini Yesu, baada ya kuwaita, akawaambia: “Mnajua kwamba wale ambao huonekana kuwa wanatawala mataifa hupiga ubwana juu yao na wakuu wao hutumia mamlaka juu yao.+
5 Vivyo hivyo, enyi vijana, jitiisheni+ kwa wanaume wazee. Lakini ninyi nyote jifungeni unyenyekevu wa akili kuelekeana ninyi wenyewe,+ kwa sababu Mungu huwapinga wenye majivuno, lakini huwapa wanyenyekevu fadhili zisizostahiliwa.+