Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 33:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Tafadhali, ichukue zawadi ya baraka yangu iliyoletwa kwako,+ kwa sababu Mungu amenipa kibali na kwa sababu nina kila kitu.”+ Naye akaendelea kumhimiza, hata akaichukua.+

  • 1 Samweli 25:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Mara moja Abigaili+ akafanya haraka, akachukua mikate mia mbili na mitungi miwili mikubwa ya divai+ na kondoo watano+ na vipimo vitano vya sea vya nafaka iliyochomwa+ na keki mia moja za zabibu kavu+ na keki mia mbili za tini zilizoshinikizwa,+ akazipakia juu ya punda.

  • 1 Samweli 30:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Wakati Daudi alipofika Siklagi, akapeleka sehemu ya nyara kwa wanaume wazee wa Yuda, rafiki zake,+ akisema: “Tazameni, hii ni zawadi+ ya baraka kwa ajili yenu kutoka katika nyara za adui za Yehova.”

  • 2 Wafalme 5:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Ndipo akarudi kwa yule mtu wa Mungu wa kweli,+ yeye na kambi yake yote, akaenda, akasimama mbele yake na kusema: “Tazama, sasa, hakika ninajua kwamba hakuna Mungu yeyote mahali pengine popote duniani isipokuwa katika Israeli.+ Na sasa, tafadhali pokea zawadi ya kubariki+ kutoka kwa mtumishi wako.”

  • Methali 18:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Zawadi ya mwanadamu itamfungulia nafasi kubwa,+ nayo itamwongoza hata mbele ya watu wakuu.+

  • Methali 25:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Ikiwa mtu anayekuchukia ana njaa, mpe mkate ale; na ikiwa ana kiu, mpe maji anywe.+

  • Methali 25:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Kwa maana unakusanya makaa ya moto juu ya kichwa chake,+ na Yehova mwenyewe atakupa thawabu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki