Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 25:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Nao watanifanyia patakatifu, kwa maana mimi nitakaa katikati yao.+

  • Kutoka 40:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Katika siku ya mwezi wa kwanza,+ siku ya kwanza ya mwezi, utaisimamisha maskani ya hema la mkutano.+

  • 1 Samweli 1:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Kwa hiyo mara tu alipomwachisha kunyonya, akapanda pamoja naye, pamoja na ng’ombe-dume wa miaka mitatu na efa moja ya unga na mtungi mkubwa wa divai,+ naye akaingia ndani ya nyumba ya Yehova katika Shilo.+ Na huyo mvulana alikuwa pamoja naye.

  • 1 Samweli 3:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Na taa ya Mungu ilikuwa haijazimwa bado, na Samweli alikuwa amelala katika hekalu+ la Yehova, palipokuwa sanduku la Mungu.

  • 2 Samweli 7:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 ndipo mfalme alipomwambia Nathani+ nabii: “Tazama, mimi ninakaa katika nyumba ya mierezi,+ lakini sanduku la Mungu wa kweli linakaa katikati ya vitambaa vya mahema.”+

  • 2 Samweli 22:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Katika taabu yangu niliendelea kumwita Yehova,+

      Nami niliendelea kumwita Mungu wangu.+

      Ndipo kutoka katika hekalu lake akaisikia sauti yangu,+

      Kilio changu cha kuomba msaada kikaingia masikioni mwake.+

  • Zaburi 27:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Nimemwomba Yehova jambo moja+—

      Ndilo nitakalolitafuta,+

      Kwamba nipate kukaa katika nyumba ya Yehova siku zote za maisha yangu,+

      Ili kuuona uzuri wa Yehova+

      Na kulitazama kwa uthamini hekalu lake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki