Zaburi
Ya Daudi.
27 Yehova ni nuru yangu+ na wokovu wangu.+
2 Watenda-maovu walipokuja karibu juu
yangu ili wapate kuila nyama yangu,+
Wao wakiwa ni wapinzani wangu na adui zangu,+
Wao walijikwaa na kuanguka.+
3 Hata kambi ijapopiga hema dhidi yangu,+
Moyo wangu hautaogopa.+
Vita vijapozuka dhidi yangu,+
Bado nitakuwa na tegemeo wakati huo.+
4 Nimemwomba Yehova jambo moja+—
Ndilo nitakalolitafuta,+
Kwamba nipate kukaa katika nyumba ya Yehova siku zote za maisha yangu,+
Ili kuuona uzuri wa Yehova+
Na kulitazama kwa uthamini hekalu lake.+
5 Kwa maana atanificha mafichoni mwake katika siku ya msiba;+
Atanificha katika mahali pa siri pa hema lake;+
Ataniweka juu kwenye mwamba.+
6 Na sasa kichwa changu kitakuwa juu, juu ya adui zangu wanaonizunguka pande zote;+
Nami nitatoa kwenye hema lake dhabihu za vigelegele vya shangwe;+
Nitamwimbia Yehova na kumpigia muziki.+
Usimgeuzie mbali mtumishi wako kwa hasira.+
Uwe msaada wangu.+
Usinitupe wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu.+
12 Usinitie mikononi mwa nafsi ya wapinzani wangu;+
Kwa maana dhidi yangu wamesimama mashahidi wa uwongo,+
Na yeye anayetokeza jeuri.+
13 Kama nisingalikuwa na imani katika kuuona wema wa Yehova katika nchi ya walio hai+—!