2 Samweli
22 Na Daudi akamwambia Yehova maneno ya wimbo+ huu siku ambayo Yehova alikuwa amemkomboa kutoka katika mkono wa adui+ zake wote na kutoka katika mkono wa Sauli;+ 2 naye akasema:
“Yehova ni mwamba+ wangu na ngome+ yangu na Mwokoaji wangu.+
3 Mungu wangu ni mwamba+ wangu. Nitamkimbilia,
Ngao+ yangu na pembe+ yangu ya wokovu, kilele+ changu salama,
Na mahali pangu pa kukimbilia,+ Mwokozi+ wangu; unaniokoa kutoka katika jeuri.+
5 Kwa maana mashuu yanayosababisha kifo yalinizunguka;+
Kulikuwa na mafuriko ya ghafula ya watu wasiofaa kitu yaliyoendelea kuniogopesha.+
7 Katika taabu yangu niliendelea kumwita Yehova,+
Nami niliendelea kumwita Mungu wangu.+
Ndipo kutoka katika hekalu lake akaisikia sauti yangu,+
Kilio changu cha kuomba msaada kikaingia masikioni mwake.+
8 Nayo dunia ikaanza kutikisika na kutetemeka;+
Misingi ya mbingu ikasukasuka,+
Nayo ikatikisika-tikisika kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+
9 Moshi ukapanda katika mianzi ya pua yake, na moto kutoka kinywani mwake ukaendelea kuteketeza;+
Makaa yakawaka moto kutoka kwake.+
11 Naye akaja akiwa amepanda juu ya kerubi,+ akaja akiwa anaruka;
Naye akaonekana juu ya mabawa ya roho.+
13 Kutoka katika mwangaza mbele yake yakawaka makaa yanayowaka ya moto.+
16 Na sakafu za vijito vya bahari zikaonekana,+
Misingi ya nchi yenye kuzaa+ ikafunuliwa,
Kwa kemeo la Yehova, kwa mlipuko wa pumzi ya pua yake.+
18 Alikuwa akinikomboa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+
Kutoka kwa wale wanaonichukia; kwa sababu walikuwa na nguvu kuliko mimi.+
20 Naye akanitoa nje mpaka mahali penye nafasi tele;+
Alikuwa akiniokoa, kwa sababu alikuwa amependezwa nami.+
23 Kwa maana maamuzi yake yote ya hukumu+ yako mbele yangu;
Na kwa habari ya sheria zake, sitageuka kando kuziacha.+
26 Kwa mtu mshikamanifu utatenda kwa ushikamanifu;+
Kwa mtu asiye na kosa, mwenye nguvu, utatenda kwa njia isiyo na kosa;+
30 Kwa maana kwa msaada wako ninaweza kukimbiza kikundi cha waporaji;+
Kwa msaada wa Mungu wangu ninaweza kuupanda ukuta.+
31 Mungu wa kweli, njia yake ni kamilifu;+
Neno la Yehova limetakaswa.+
Yeye ni ngao kwa wale wote wanaomkimbilia.+
34 Anaifanya miguu yangu iwe kama ile ya paa;+
Na kwenye mahali palipo juu kwa ajili yangu yeye huendelea kunisimamisha.+
37 Utafanyiza nafasi kubwa ya kutosha kwa ajili ya hatua zangu zilizo chini yangu;+
Navyo vifundo vya miguu yangu hakika havitatetemeka.+
39 Nami nitawaangamiza na kuwavunja vipande-vipande,+ ili wasisimame;+
Nao wataanguka chini ya miguu yangu.+
41 Nao adui zangu, utanipa upande wa nyuma wa shingo yao;+
Wale wanaonichukia vikali—nitawanyamazisha pia.+
43 Nami nitawatwanga wawe laini kama mavumbi ya udongo;
Nitawaponda kama matope ya barabarani;+
Nitawapiga niwalaze.
44 Nawe utanifanya niponyoke lawama ya watu wangu.+
Utanilinda niwe kiongozi wa mataifa;+
Watu ambao sikujua—watanitumikia.+
48 Mungu wa kweli ndiye Mpaji wa matendo ya kisasi kwangu+
Na ndiye anayeshusha vikundi vya watu chini yangu,+