Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waamuzi 14:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Lakini baba yake na mama yake wakamwambia: “Je, hakuna mwanamke yeyote kati ya binti za ndugu zako na kati ya watu wangu wote,+ hivi kwamba uende kumchukua mwanamke kutoka kwa Wafilisti wasiotahiriwa?”+ Lakini bado Samsoni akamwambia baba yake: “Nileteeni huyo, kwa maana ndiye anayestahili kabisa machoni pangu.”

  • 1 Samweli 17:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Na Daudi akaanza kuwaambia watu waliokuwa wamesimama karibu naye: “Atafanyiwa nini mtu atakayempiga yule Mfilisti+ pale na kuondolea mbali shutuma kutoka juu ya Israeli?+ Kwani huyu Mfilisti asiyetahiriwa+ ni nani hata avitukane+ vikosi vya Mungu aliye hai?”+

  • 1 Samweli 17:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Mtumishi wako alimuua simba na dubu vilevile; na huyu Mfilisti+ asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wa hao, kwa kuwa amevitukana+ vikosi+ vya Mungu aliye hai.”+

  • 1 Samweli 21:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Nao watumishi wa Akishi wakaanza kumwambia: “Je, huyu si Daudi mfalme+ wa ile nchi? Je, haikuwa kwa huyu ambaye waliendelea kuitikia kwa kucheza dansi,+ wakisema,

      ‘Sauli amepiga maelfu yake,

      Na Daudi makumi ya maelfu yake’?”+

  • 2 Samweli 1:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Msiseme hayo katika Gathi;+

      Msiyatangaze katika barabara za Ashkeloni,+

      Binti za Wafilisti wasije wakashangilia,

      Binti za watu wasiotahiriwa wasije wakafurahi.+

  • 2 Samweli 3:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Zaidi ya hayo, Daudi akatuma wajumbe kwa Ish-boshethi,+ mwana wa Sauli, akisema: “Mtoe mke wangu Mikali, niliyemchumbia kwa magovi+ mia moja ya Wafilisti.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki