Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 34:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Nao wakaendelea kuwaambia: “Sisi hatuwezi kamwe kufanya jambo la namna hiyo, kumpa mwanamume mwenye govi+ dada yetu, kwa sababu hilo ni shutuma kwetu.

  • 1 Samweli 14:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Basi Yonathani akamwambia yule mtumishi, mchukua-silaha wake: “Haya njoo, na tuvuke, twende kwenye kituo cha mbele cha wanaume hawa wasiotahiriwa.+ Labda Yehova atatenda kwa ajili yetu, kwa maana hakuna kizuizi chochote kwa Yehova kuokoa kwamba ni kwa wengi au ni kwa wachache.”+

  • 1 Samweli 17:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Na Daudi akaanza kuwaambia watu waliokuwa wamesimama karibu naye: “Atafanyiwa nini mtu atakayempiga yule Mfilisti+ pale na kuondolea mbali shutuma kutoka juu ya Israeli?+ Kwani huyu Mfilisti asiyetahiriwa+ ni nani hata avitukane+ vikosi vya Mungu aliye hai?”+

  • 1 Samweli 31:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Ndipo Sauli akamwambia mchukua-silaha wake: “Chomoa upanga wako,+ unichome nao, ili watu hawa wasiotahiriwa+ wasije na kunichoma na kunitendea vibaya.” Naye mchukua-silaha wake hakutaka,+ kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akachukua upanga, akauangukia.+

  • 2 Samweli 1:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Msiseme hayo katika Gathi;+

      Msiyatangaze katika barabara za Ashkeloni,+

      Binti za Wafilisti wasije wakashangilia,

      Binti za watu wasiotahiriwa wasije wakafurahi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki