Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 17:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Hili ndilo agano langu ambalo ninyi mtashika, kati yangu na ninyi, hata uzao wako baada yako.+ Kila mwanamume wa kwenu lazima atahiriwe.+

  • Waamuzi 14:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Lakini baba yake na mama yake wakamwambia: “Je, hakuna mwanamke yeyote kati ya binti za ndugu zako na kati ya watu wangu wote,+ hivi kwamba uende kumchukua mwanamke kutoka kwa Wafilisti wasiotahiriwa?”+ Lakini bado Samsoni akamwambia baba yake: “Nileteeni huyo, kwa maana ndiye anayestahili kabisa machoni pangu.”

  • Waamuzi 15:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Kisha akawa na kiu sana, na kuanza kumwita Yehova, akisema: “Wewe ndiye uliyetia wokovu huu mkubwa mkononi mwa mtumishi wako,+ na je, sasa nife kutokana na kiu, na je, nianguke mkononi mwa wasiotahiriwa?”+

  • 1 Samweli 17:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Mtumishi wako alimuua simba na dubu vilevile; na huyu Mfilisti+ asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wa hao, kwa kuwa amevitukana+ vikosi+ vya Mungu aliye hai.”+

  • 2 Samweli 1:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Msiseme hayo katika Gathi;+

      Msiyatangaze katika barabara za Ashkeloni,+

      Binti za Wafilisti wasije wakashangilia,

      Binti za watu wasiotahiriwa wasije wakafurahi.+

  • 1 Mambo ya Nyakati 10:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Ndipo Sauli akamwambia mchukua-silaha wake:+ “Chomoa upanga wako,+ unichome nao, ili watu hawa wasiotahiriwa+ wasije kunitendea vibaya.”+ Naye mchukua-silaha wake hakutaka,+ kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akachukua upanga, akauangukia.+

  • Yeremia 9:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 juu ya Misri+ na juu ya Yuda+ na juu ya Edomu+ na juu ya wana wa Amoni+ na juu ya Moabu+ na juu ya wote wenye nywele zilizokatwa kwenye vipaji vya nyuso wanaokaa nyikani;+ kwa maana mataifa yote hayakutahiriwa, na nyumba yote ya Israeli hawakutahiriwa moyoni.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki