6 Ndipo Yoshua akararua nguo zake za kujitanda, akaanguka kifudifudi+ mbele ya sanduku la Yehova mpaka jioni, yeye na wanaume wazee wa Israeli, nao wakawa wakitia mavumbi vichwani mwao.+
4Basi Mordekai+ akapata kujua mambo yote yaliyokuwa yamefanywa;+ ndipo Mordekai akararua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia+ na majivu,+ akaenda katikati ya jiji, akalia kwa sauti kubwa na yenye uchungu.+
26 Ee binti ya watu wangu, vaa nguo ya gunia+ na ugaegae katika majivu.+ Omboleza kama kumwombolezea mwana wa pekee, kilio cha uchungu;+ kwa sababu mporaji atakuja juu yetu kwa ghafula.+