-
1 Wafalme 12:32Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
32 Na Yeroboamu akafanya sherehe katika mwezi wa nane siku ya kumi na tano ya mwezi huo, kama ile sherehe iliyokuwa katika Yuda,+ ili atoe matoleo juu ya madhabahu aliyokuwa ameijenga kule Betheli, ya kutoa dhabihu kwa wale ndama aliotengeneza; naye akaweka makuhani Betheli+ wahudumu mahali pa juu alipokuwa amejenga.
-
-
1 Wafalme 14:10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 kwa sababu hiyo tazama, nitaleta msiba juu ya nyumba ya Yeroboamu, nami kwa hakika nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu yeyote anayekojoa ukutani,+ asiye na uwezo na asiye na thamani katika Israeli;+ nami kwa kweli nitafagia kabisa nikiifuata nyumba ya Yeroboamu,+ kama vile mtu anavyoondoa mavi mpaka yanapokuwa yameondolewa.+
-