Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 11:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Naye akamwambia Yeroboamu:

      “Chukua wewe vipande kumi; kwa maana Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Tazama, ninaurarua ufalme kutoka mkononi mwa Sulemani, nami hakika nitakupa wewe makabila kumi.+

  • 1 Wafalme 12:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Na ikawa kwamba mara tu Yeroboamu+ mwana wa Nebati aliposikia habari hizo alipokuwa angali Misri (kwa maana alikuwa amekimbia kwa sababu ya Mfalme Sulemani, ili Yeroboamu akae Misri),+

  • 1 Wafalme 12:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Na Yeroboamu akafanya sherehe katika mwezi wa nane siku ya kumi na tano ya mwezi huo, kama ile sherehe iliyokuwa katika Yuda,+ ili atoe matoleo juu ya madhabahu aliyokuwa ameijenga kule Betheli, ya kutoa dhabihu kwa wale ndama aliotengeneza; naye akaweka makuhani Betheli+ wahudumu mahali pa juu alipokuwa amejenga.

  • 1 Wafalme 14:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 kwa sababu hiyo tazama, nitaleta msiba juu ya nyumba ya Yeroboamu, nami kwa hakika nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu yeyote anayekojoa ukutani,+ asiye na uwezo na asiye na thamani katika Israeli;+ nami kwa kweli nitafagia kabisa nikiifuata nyumba ya Yeroboamu,+ kama vile mtu anavyoondoa mavi mpaka yanapokuwa yameondolewa.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 11:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kwa maana Walawi waliviacha viwanja vyao vya malisho+ na miliki+ yao kisha wakaja Yuda na Yerusalemu,+ kwa sababu Yeroboamu+ na wanawe walikuwa wamewaondoa+ wasiwe makuhani kwa Yehova.

  • 2 Mambo ya Nyakati 13:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Basi Abiya akaingia vitani na jeshi la wanaume wenye nguvu wa vita,+ mia nne elfu, wanaume waliochaguliwa. Naye Yeroboamu akajipanga kivita kupigana naye akiwa na wanaume waliochaguliwa mia nane elfu, mashujaa, wanaume wenye nguvu.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 13:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Na Yeroboamu hakuwa na nguvu+ tena katika siku za Abiya; lakini Yehova akampiga,+ hivi kwamba akafa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki