16 Lakini waliendelea kuwadhihaki+ wale wajumbe wa Mungu wa kweli na kuyadharau maneno+ yake na kuwafanyia mzaha+ manabii wake, mpaka ghadhabu+ ya Yehova ikapanda juu ya watu wake, mpaka kukawa hakuna kuponywa.+
14 Watenda-dhambi wamekuwa na hofu katika Sayuni;+ mtetemeko umewashika waasi-imani:+ ‘Ni nani kati yetu anayeweza kukaa kwa muda na moto unaoteketeza?+ Ni nani kati yetu anayeweza kukaa kwa muda wowote pamoja na mioto inayodumu muda mrefu?’+
20 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama! Hasira yangu na ghadhabu yangu zinamwagwa juu ya mahali hapa,+ juu ya mwanadamu na juu ya mnyama wa kufugwa, na juu ya mti wa shambani+ na juu ya mazao ya udongo; nayo itateketeza, wala haitazimwa.’+
27 “‘“Lakini ikiwa hamtanitii kwa kuitakasa siku ya sabato na kutobeba mzigo,+ lakini mwingie nao kupitia malango ya Yerusalemu katika siku ya sabato, mimi pia nitawasha moto wa kuteketeza katika malango yake,+ nao hakika utaiteketeza minara ya makao ya Yerusalemu+ nao hautazimwa.”’”+