Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 32:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Wamegeuka kando haraka kutoka katika njia niliyowaamuru waende.+ Wamejifanyia sanamu ya kuyeyushwa ya ndama na wanaendelea kuiinamia na kuitolea dhabihu na kusema, ‘Huyu ndiye Mungu wako, Ee Israeli, aliyekuongoza kutoka nchi ya Misri.’”+

  • 1 Samweli 12:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Basi Samweli akawaambia watu: “Msiogope.+ Ninyi—mmefanya uovu huu wote. Ila tu msigeuke kando mwache kumtumikia Yehova,+ nanyi lazima mmtumikie Yehova kwa moyo wenu wote.+

  • Zaburi 97:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Enyi mnaompenda Yehova,+ chukieni yaliyo mabaya.+

      Yeye anazilinda nafsi za washikamanifu wake;+

      Huwakomboa kutoka katika mkono wa waovu.+

  • Zaburi 119:128
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 128 Ndiyo sababu nimeyaona maagizo yote juu ya mambo yote kuwa ni sawa;+

      Nimechukia kila njia ya uwongo.+

  • Methali 8:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kumwogopa Yehova humaanisha kuchukia yaliyo mabaya.+ Nimechukia kujiinua na kiburi+ na njia mbaya na kinywa kipotovu.+

  • Methali 13:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Mwadilifu huchukia neno la uwongo,+ lakini waovu hutenda kwa aibu na kujiletea fedheha.+

  • Sefania 1:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 na wale wanaorudi nyuma wasimfuate Yehova,+ ambao hawakumtafuta Yehova wala kuuliza habari kutoka kwake.”+

  • Waroma 12:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Upendo+ wenu na uwe bila unafiki.+ Chukieni maovu,+ shikamaneni na mema.+

  • Waebrania 1:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Uliupenda uadilifu, nawe ukauchukia uasi-sheria. Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, alikutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia kuliko wenzako.”+

  • Waebrania 10:38
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 38 “Lakini mwadilifu wangu ataishi kwa sababu ya imani,”+ na, “akirudi nyuma kwa kutetemeka, nafsi yangu haipendezwi naye.”+

  • 2 Petro 2:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Kwa maana ingalikuwa afadhali kwao kama hawangalijua kwa usahihi njia ya uadilifu+ kuliko baada ya kuijua kwa usahihi kugeuka kutoka katika amri takatifu waliyopewa.+

  • Yuda 23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 waokoeni+ kwa kuwanyakua kutoka katika moto.+ Lakini endeleeni kuonyesha wengine rehema, mkifanya hivyo kwa kuogopa, huku mkilichukia hata vazi la ndani ambalo mwili umelitia doa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki