Methali
13 Mwana ni mwenye hekima palipo na nidhamu ya baba,+ lakini mtu mwenye dhihaka ni yule ambaye hajasikia kemeo.+
2 Kutokana na matunda ya kinywa chake, mtu atakula mema,+ lakini nafsi ya wale wanaotenda kwa hila ni ujeuri.+
3 Anayelinda kinywa chake anaitunza nafsi yake.+ Anayefungua wazi midomo yake—yeye atapata uharibifu.+
4 Mvivu anajionyesha kutamani, lakini nafsi yake haina chochote.+ Hata hivyo, nafsi ya wenye bidii itanoneshwa.+
5 Mwadilifu huchukia neno la uwongo,+ lakini waovu hutenda kwa aibu na kujiletea fedheha.+
6 Uadilifu humlinda mtu asiye na lawama katika njia yake,+ lakini uovu humpindua mtenda-dhambi.+
7 Kuna mtu anayejifanya kuwa tajiri lakini hana chochote;+ kuna mtu anayejifanya kuwa maskini lakini ana vitu vingi vyenye thamani.
8 Fidia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake,+ lakini maskini hajasikia kemeo.+
9 Nuru ya waadilifu itashangilia;+ lakini taa ya waovu—hiyo itazimwa.+
10 Kwa sababu ya kimbelembele mtu husababisha tu pambano,+ lakini wale wanaoshauriana pamoja wana hekima.+
11 Vitu vyenye thamani vinavyopatikana kwa ubatili hupungua,+ lakini mtu anayekusanya kwa mkono ndiye anayepata ongezeko.+
12 Tarajio lililocheleweshwa linafanya moyo uwe mgonjwa,+ lakini kitu kinachotamaniwa kinapokuja ni mti wa uzima.+
13 Yule ambaye amelidharau neno,+ atadaiwa rehani ya mtu mwenye deni; lakini mtu anayeiogopa amri ndiye atakayepewa thawabu.+
14 Sheria ya mwenye hekima ni chemchemi ya uzima,+ ili kumwepusha mtu na mitego ya kifo.+
15 Ufahamu mzuri huleta kibali,+ lakini njia ya wale wanaotenda kwa hila ni ngumu.+
16 Kila mtu aliye mwerevu atatenda kwa ujuzi,+ lakini mjinga ataeneza upumbavu kila mahali.+
17 Mjumbe mwovu ataanguka katika jambo baya,+ lakini mjumbe mwaminifu huponya.+
18 Anayepuuza nidhamu hupatwa na umaskini na aibu,+ lakini anayeshika karipio ndiye anayetukuzwa.+
19 Tamaa inapotimizwa inafurahisha nafsi;+ lakini kuepuka yaliyo mabaya ni chukizo kwa wajinga.+
20 Anayetembea na watu wenye hekima atakuwa na hekima,+ lakini anayeshirikiana na wajinga atapatwa na mabaya.+
21 Watenda-dhambi ndio hufuatwa na msiba,+ lakini waadilifu ndio ambao wema huwapa thawabu.+
22 Mtu mwema atawaachia urithi wana wa wanawe, na mali ya mtenda-dhambi huwekwa akiba kwa ajili ya mwadilifu.+
23 Udongo uliolimwa wa watu maskini hutoa chakula kingi,+ lakini kuna mtu anayefagiliwa mbali kwa sababu ya ukosefu wa hukumu.+
24 Anayezuia fimbo yake anamchukia mwana wake,+ lakini anayempenda ni yule anayemwangalia kwa nidhamu.+
25 Mwadilifu anakula mpaka nafsi yake inaposhiba,+ lakini tumbo la waovu litakuwa tupu.+