3 Nawe mwenyewe hutaponyoka kutoka mkononi mwake, kwa sababu bila shaka utakamatwa na kutiwa mkononi mwake.+ Na macho yako yatayaona macho ya mfalme wa Babiloni,+ na kinywa chake kitasema na kinywa chako, nawe utaenda Babiloni.’
17 Na Mfalme Sedekia akatuma watu kumchukua, na mfalme akaanza kumuuliza maswali katika nyumba yake mahali pa maficho.+ Naye akaendelea kusema: “Je, liko neno lolote kutoka kwa Yehova?” Yeremia akasema: “Liko!” Naye akaendelea kusema: “Utatiwa mkononi mwa mfalme wa Babiloni!”+
18 Lakini ikiwa hutaenda nje kwa wakuu wa mfalme wa Babiloni, jiji hili pia lazima litatiwa mkononi mwa Wakaldayo, nao kwa kweli wataliteketeza kwa moto,+ nawe hutaponyoka mkononi mwao.’”+
5 Na jeshi la Wakaldayo likawafuatilia,+ nao wakamfikia Sedekia katika nchi tambarare ya jangwa la Yeriko.+ Kisha wakamchukua na kumleta kwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi+ ili atangaze hukumu juu yake.+
13 Nami nitautandaza wavu wangu juu yake, naye atakamatwa katika wavu wangu wa kuwindia;+ nami nitampeleka Babiloni, mpaka nchi ya Wakaldayo,+ lakini hataiona; naye atakufa huko.+