25 Ndipo watalazimika kusema, ‘Ni kwa sababu waliliacha agano+ la Yehova Mungu wa mababu zao, ambalo alifanya pamoja nao alipowatoa katika nchi ya Misri.+
12 Hivyo wakamwacha Yehova Mungu wa baba zao aliyekuwa amewatoa katika nchi ya Misri,+ wakafuata miungu mingine kutoka kati ya miungu ya watu waliowazunguka pande zote,+ wakaanza kuiinamia, hata wakamtia uchungu Yehova.+
26 “Hata hivyo, wakakosa kutii,+ wakakuasi+ na kuzidi kutupa sheria yako nyuma ya migongo yao,+ wakawaua manabii wako mwenyewe,+ waliotoa ushahidi juu yao ili kuwarudisha kwako;+ nao wakaendelea kutenda matendo ya ukosefu mkubwa wa heshima.+
8 Makuhani wenyewe hawakusema, ‘Yehova yuko wapi?’+ Na wale wanaoshughulika na sheria hawakunijua;+ na wachungaji wenyewe walinikosea,+ na hata manabii walitoa unabii kupitia Baali,+ nao wakawafuata wale ambao hawangeweza kuleta faida yoyote.+
7 Nawezaje kukusamehe kwa ajili ya jambo hili? Wana wako wameniacha, nao wanaendelea kuapa+ kwa kitu ambacho si Mungu.+ Nami niliendelea kuwashibisha,+ lakini wakaendelea kufanya uzinzi,+ nao wanaenda katika nyumba ya mwanamke kahaba wakiwa makundi-makundi.