Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 29:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Ndipo watalazimika kusema, ‘Ni kwa sababu waliliacha agano+ la Yehova Mungu wa mababu zao, ambalo alifanya pamoja nao alipowatoa katika nchi ya Misri.+

  • Waamuzi 2:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Hivyo wakamwacha Yehova Mungu wa baba zao aliyekuwa amewatoa katika nchi ya Misri,+ wakafuata miungu mingine kutoka kati ya miungu ya watu waliowazunguka pande zote,+ wakaanza kuiinamia, hata wakamtia uchungu Yehova.+

  • Nehemia 9:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 “Hata hivyo, wakakosa kutii,+ wakakuasi+ na kuzidi kutupa sheria yako nyuma ya migongo yao,+ wakawaua manabii wako mwenyewe,+ waliotoa ushahidi juu yao ili kuwarudisha kwako;+ nao wakaendelea kutenda matendo ya ukosefu mkubwa wa heshima.+

  • Yeremia 2:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Makuhani wenyewe hawakusema, ‘Yehova yuko wapi?’+ Na wale wanaoshughulika na sheria hawakunijua;+ na wachungaji wenyewe walinikosea,+ na hata manabii walitoa unabii kupitia Baali,+ nao wakawafuata wale ambao hawangeweza kuleta faida yoyote.+

  • Yeremia 5:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Nawezaje kukusamehe kwa ajili ya jambo hili? Wana wako wameniacha, nao wanaendelea kuapa+ kwa kitu ambacho si Mungu.+ Nami niliendelea kuwashibisha,+ lakini wakaendelea kufanya uzinzi,+ nao wanaenda katika nyumba ya mwanamke kahaba wakiwa makundi-makundi.

  • Yeremia 22:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Nao watasema: “Kwa sababu wameliacha agano la Yehova Mungu+ wao na kuinamia miungu mingine na kuitumikia.”’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki