14 Na hakika mtu atauvunja kama vile mtungi mkubwa wa wafinyanzi unavyovunjwa,+ kupondwa vipande-vipande bila mtu kuuachilia, hivi kwamba kati ya vipande vyake vilivyopondwa hakuwezi kupatikana kigae kinachoweza kutumiwa kukusanya moto jikoni wala kuteka maji kutoka eneo lenye matope.”+
11 Nawe uwaambie, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Ndivyo nitakavyowavunja watu hawa na jiji hili kama mtu anavyokivunja chombo cha mfinyanzi hivi kwamba hakiwezi kurekebishwa tena;+ nao watazika katika Tofethi+ mpaka pasiwe na mahali zaidi pa kuzikia.”’+
28 Je, mtu huyu Konia+ ni umbo tu lililodharauliwa, lililovunjwa vipande-vipande,+ au ni chombo ambacho hakipendezi?+ Kwa nini yeye na uzao wake ni lazima waangushwe chini na kutupwa katika nchi ambayo hawakuijua?’+