Maombolezo
5 Ee Yehova, ukumbuke yale yaliyotupata.+ Utazame, uone shutuma zetu.+
2 Fungu la urithi wetu limeenda kwa wageni, nyumba zetu kwa watu wa kutoka ugenini.+
3 Tumekuwa mayatima wasio na baba.+ Mama zetu ni kama wajane.+
4 Tumetumia pesa ili tunywe maji yetu wenyewe.+ Kuni zetu wenyewe zinatujia kwa bei.
5 Tumefuatiwa kwa ukaribu kwenye shingo zetu.+ Tumechoka. Hatukuachiwa pumziko lolote.+
6 Tumewapa mkono+ Misri;+ Ashuru,+ ili tushibe mkate.
7 Mababu zetu ndio wamefanya dhambi.+ Hawako tena. Lakini sisi, imekuwa lazima tuchukue makosa yao.+
8 Watumishi wametawala juu yetu.+ Hakuna anayetunyakua kutoka mkononi mwao.+
9 Tunauleta mkate wetu kwa kuhatarisha nafsi zetu,+ kwa sababu ya upanga wa nyika.
10 Ngozi yetu imekuwa moto kama tanuru, kwa sababu ya maumivu ya njaa.+
11 Wake wamenyenyekezwa katika Sayuni,+ mabikira katika majiji ya Yuda.
12 Wakuu wametundikwa kwa mkono wao.+ Hata nyuso za wanaume wazee hazikuheshimiwa.+
13 Hata vijana wameinua jiwe la kusagia la mkononi,+ na wavulana wamejikwaa chini ya kuni.+
14 Wanaume wazee wameacha kutoka langoni,+ vijana wamekomesha muziki wao wa vyombo.+
15 Furaha ya moyo wetu imekoma. Mchezo wetu wa dansi umebadilishwa uwe maombolezo matupu.+
16 Taji la kichwa chetu limeanguka.+ Ole wetu, sasa, kwa sababu tumefanya dhambi!+
17 Kwa sababu hiyo moyo wetu umekuwa mgonjwa.+ Kwa sababu ya mambo haya macho yetu yameingia giza,+
18 Kwa sababu ya mlima wa Sayuni ambao umefanywa ukiwa;+ mbweha wametembea juu yake.+
19 Lakini wewe, Ee Yehova, utaketi mpaka wakati usio na kipimo.+ Kiti chako cha ufalme ni cha kizazi baada ya kizazi.+
20 Kwa nini unatusahau milele,+ hivi kwamba unatuacha kwa siku nyingi?+
21 Uturudishe kwako,+ Ee Yehova, nasi tutarudi bila kukawia. Utuletee siku zilizo mpya kama katika zamani za kale.+