Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 18:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Na Yehova akaendelea kumwambia Haruni: “Katika nchi yao hutakuwa na urithi, wala hakuna fungu lolote litakalokuwa lako katikati yao.+ Mimi ni fungu lako na urithi wako katikati ya wana wa Israeli.+

  • Kumbukumbu la Torati 10:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Ndiyo sababu Lawi hana fungu na urithi pamoja na ndugu zake.+ Yehova ndiye urithi wake, kama vile Yehova Mungu wako alivyokuwa amemwambia.+

  • Kumbukumbu la Torati 18:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Hakuna fungu au urithi pamoja na Israeli litakalokuja kuwa la makuhani, Walawi,+ kabila zima la Lawi. Matoleo yanayotolewa kwa njia ya moto kwa Yehova, naam, urithi wake, watayala.+

  • Yoshua 13:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kabila la Walawi peke yake ndilo ambalo hakulipatia urithi.+ Matoleo ya Yehova Mungu wa Israeli yaliyotolewa kwa njia ya moto+ ndiyo urithi wao,+ kama vile ambavyo amewaahidi.+

  • Yoshua 13:33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Lakini Musa hakuwapa urithi kabila la Walawi.+ Yehova Mungu wa Israeli ndiye urithi wao, kama vile ambavyo amewaahidi.+

  • Ezekieli 45:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Litakuwa fungu takatifu kutoka katika nchi kwa ajili ya makuhani wenyewe,+ wahudumu wa patakatifu, wale wanaokaribia ili kumhudumia Yehova.+ Na hapo patakuwa mahali pa nyumba kwa ajili yao, na mahali patakatifu kwa ajili ya patakatifu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki