20 Na Yehova akaendelea kumwambia Haruni: “Katika nchi yao hutakuwa na urithi, wala hakuna fungu lolote litakalokuwa lako katikati yao.+ Mimi ni fungu lako na urithi wako katikati ya wana wa Israeli.+
18“Hakuna fungu au urithi pamoja na Israeli litakalokuja kuwa la makuhani, Walawi,+ kabila zima la Lawi. Matoleo yanayotolewa kwa njia ya moto kwa Yehova, naam, urithi wake, watayala.+
14 Kabila la Walawi peke yake ndilo ambalo hakulipatia urithi.+ Matoleo ya Yehova Mungu wa Israeli yaliyotolewa kwa njia ya moto+ ndiyo urithi wao,+ kama vile ambavyo amewaahidi.+
4 Litakuwa fungu takatifu kutoka katika nchi kwa ajili ya makuhani wenyewe,+ wahudumu wa patakatifu, wale wanaokaribia ili kumhudumia Yehova.+ Na hapo patakuwa mahali pa nyumba kwa ajili yao, na mahali patakatifu kwa ajili ya patakatifu.