Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 23:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 “Yaliyo bora zaidi kati ya matunda ya kwanza yaliyoiva ya udongo wako utayaleta katika nyumba ya Yehova Mungu wako.+

      “Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.+

  • Hesabu 3:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kwa maana kila mzaliwa wa kwanza ni wangu.+ Katika siku niliyompiga na kumuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri+ nilijitakasia kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli kuanzia mwanadamu mpaka mnyama.+ Wanapaswa kuwa wangu. Mimi ni Yehova.”

  • Hesabu 18:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “Vyote vilivyo bora katika mafuta na vyote vilivyo bora katika divai mpya na nafaka, matunda yao ya kwanza,+ ambayo watampa Yehova, nimekupa wewe.+

  • Hesabu 18:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Na utahesabiwa kwenu kuwa mchango wenu, kama ile nafaka ya uwanja wa kupuria+ na kama yale mazao kamili ya shinikizo la divai au la mafuta.

  • Kumbukumbu la Torati 18:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Sehemu ya kwanza ya nafaka yako, divai yako mpya na mafuta yako na sufu yako ya kwanza iliyokatwa ya kundi lako unapaswa kumpa.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 31:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Tena akawaambia watu, wakaaji wa Yerusalemu, kwamba watoe fungu la makuhani+ na la Walawi,+ ili waishike+ kabisa sheria ya Yehova.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 31:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Ndipo Azaria+ mkuu wa makuhani wa nyumba ya Sadoki+ akamwambia, ndiyo, akasema: “Tangu walipoanza kuleta mchango+ ndani ya nyumba ya Yehova kumekuwako kula na kushiba+ na kuwa na ziada kwa wingi;+ kwa kuwa Yehova mwenyewe amewabariki watu wake,+ na kilichobaki ni hiki kiasi kingi.”

  • Nehemia 10:35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 na kuleta kwenye nyumba ya Yehova matunda ya kwanza yaliyoiva ya udongo wetu+ na matunda ya kwanza yaliyoiva ya mazao yote ya kila namna ya mti,+ mwaka baada ya mwaka;

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki