-
Zaburi 45:utangulizi-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Kwa kiongozi juu ya Mayungiyungi. Ya wana wa Kora. Maskili. Wimbo wa wanawake wapendwa.
2 Kwa kweli wewe una sura nzuri kuliko wana wa binadamu.+
Uvutio umemiminwa juu ya midomo yako.+
Ndiyo sababu Mungu amekubariki mpaka wakati usio na kipimo.+
4 Na katika fahari yako endelea mpaka ufanikiwe;+
Panda kwa kutetea kweli na unyenyekevu na uadilifu,+
Na mkono wako wa kuume utakufundisha mambo yenye kuogopesha.+
5 Mishale yako ni mikali—vikundi vya watu vinaendelea kuanguka chini yako+—
Katika moyo wa adui za mfalme.+
6 Mungu ni kiti chako cha ufalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele;+
Fimbo ya enzi ya ufalme wako ni fimbo ya unyoofu.+
7 Umependa uadilifu+ nawe unachukia uovu.+
Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako,+ amekutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia+ kuliko wenzako.+
8 Mavazi yako yote ni manemane na udi na kida;+
Kutoka katika jumba kuu la mfalme la pembe,+ vinanda vimekufanya ushangilie.
9 Binti+ za wafalme wamo kati ya wanawake wako wenye thamani.
Malkia+ amesimama kwenye mkono wako wa kuume akiwa amevaa dhahabu ya Ofiri.+
14 Atapelekwa kwa mfalme akiwa na mavazi yaliyofumwa.+
Mabikira katika msafara wake ambao ni rafiki zake wanaingizwa ndani kwako.+
15 Watapelekwa kwa furaha na shangwe;
Wataingia katika jumba la mfalme.
-