Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 45:utangulizi-17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • Kwa kiongozi juu ya Mayungiyungi. Ya wana wa Kora. Maskili. Wimbo wa wanawake wapendwa.

      45 Moyo wangu umesisimuka kwa sababu ya jambo jema.+

      Ninasema: “Kazi zangu zinamhusu mfalme.”+

      Ulimi wangu na uwe kalamu+ ya mwandikaji stadi.+

       2 Kwa kweli wewe una sura nzuri kuliko wana wa binadamu.+

      Uvutio umemiminwa juu ya midomo yako.+

      Ndiyo sababu Mungu amekubariki mpaka wakati usio na kipimo.+

       3 Funga upanga+ wako kwenye paja lako, ewe mwenye nguvu,+

      Pamoja na utukufu wako na fahari yako.+

       4 Na katika fahari yako endelea mpaka ufanikiwe;+

      Panda kwa kutetea kweli na unyenyekevu na uadilifu,+

      Na mkono wako wa kuume utakufundisha mambo yenye kuogopesha.+

       5 Mishale yako ni mikali​—⁠vikundi vya watu vinaendelea kuanguka chini yako+—

      Katika moyo wa adui za mfalme.+

       6 Mungu ni kiti chako cha ufalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele;+

      Fimbo ya enzi ya ufalme wako ni fimbo ya unyoofu.+

       7 Umependa uadilifu+ nawe unachukia uovu.+

      Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako,+ amekutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia+ kuliko wenzako.+

       8 Mavazi yako yote ni manemane na udi na kida;+

      Kutoka katika jumba kuu la mfalme la pembe,+ vinanda vimekufanya ushangilie.

       9 Binti+ za wafalme wamo kati ya wanawake wako wenye thamani.

      Malkia+ amesimama kwenye mkono wako wa kuume akiwa amevaa dhahabu ya Ofiri.+

      10 Sikiliza, ewe binti, uone, na utege sikio lako;

      Na uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako.+

      11 Naye mfalme atautamani urembo wako,+

      Kwa maana yeye ni bwana wako,+

      Kwa hiyo mwinamie.+

      12 Binti Tiro na zawadi pia+—

      Walio matajiri kati ya watu watautuliza uso wako mwenyewe.+

      13 Binti ya mfalme ana utukufu wote ndani ya nyumba;+

      Mavazi yake yamepambwa kwa dhahabu.

      14 Atapelekwa kwa mfalme akiwa na mavazi yaliyofumwa.+

      Mabikira katika msafara wake ambao ni rafiki zake wanaingizwa ndani kwako.+

      15 Watapelekwa kwa furaha na shangwe;

      Wataingia katika jumba la mfalme.

      16 Mahali pa mababu+ zako patachukuliwa na wana wako,+

      Ambao utawaweka kuwa wakuu katika dunia yote.+

      17 Nitalitaja jina lako katika vizazi vyote vitakavyokuja.+

      Ndiyo sababu vikundi vya watu vitakusifu mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.

  • Mathayo 22:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Ufalme wa mbinguni umekuwa kama mtu, mfalme, aliyefanya karamu ya ndoa+ kwa ajili ya mwana wake.

  • 2 Wakorintho 11:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Kwa maana nina wivu juu yenu kwa wivu wa kimungu,+ kwa maana mimi binafsi niliwachumbia+ ninyi mume+ mmoja ili niwatoe mkiwa bikira safi kiadili+ kwa Kristo.+

  • Ufunuo 19:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Acheni tushangilie na kuwa wenye shangwe mno, na tumpe yeye utukufu,+ kwa sababu ndoa+ ya Mwana-Kondoo imefika+ na mke wake amejitayarisha.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki