Kwa kiongozi juu ya Mayungiyungi.+ Kikumbusho. Ya Asafu.+ Muziki.
80 Ee Mchungaji wa Israeli, tega sikio,+
Wewe unayemwongoza Yosefu kama kundi.+
Wewe unayeketi juu ya makerubi,+ uangaze.+
2 Mbele ya Efraimu na Benyamini na Manase, uamshe nguvu zako,+
Na uje kutuokoa.+
3 Ee Mungu, uturudishe;+
Na uutie uso wako nuru, ili tupate kuokolewa.+
4 Ee Yehova Mungu wa majeshi, utaendelea kuwaka hasira juu ya sala ya watu wako mpaka wakati gani?+
5 Umewalisha mkate wa machozi,+
Nawe unaendelea kuwafanya wanywe machozi kwa machozi kwa kiasi kikubwa.+
6 Ulituweka tugombane na jirani zetu,+
Nao adui zetu wanaendelea kudharau kama wanavyopenda.+
7 Ee Mungu wa majeshi, uturudishe;+
Na uutie uso wako nuru, ili tupate kuokolewa.+
8 Ulifanya mzabibu uondoke Misri.+
Ukaendelea kuyafukuza mataifa, ili uupande.+
9 Ulitengeneza nafasi mbele yake,+ ili upate kutia mizizi na kuijaza nchi.+
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,
Na mierezi ya Mungu kwa matawi yake.+
11 Hatua kwa hatua uliyaeneza matawi yake mpaka baharini,+
Na machipukizi yake mpaka kwenye ule Mto.+
12 Kwa nini umebomoa kuta zake za mawe,+
Na kwa nini wale wote wanaopita barabarani wameuchuma?+
13 Nguruwe-mwitu kutoka msituni anaendelea kuula,+
Na makundi ya wanyama wa porini wanaendelea kuula.+
14 Ee Mungu wa majeshi, urudi, tafadhali;+
Utazame chini kutoka mbinguni, uone na kuutunza mzabibu huu,+
15 Na shina ambalo mkono wako wa kuume umepanda,+
Na umtazame mwana ambaye umemfanya kuwa mwenye nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+
16 Huo umeteketezwa kwa moto, umekatwa.+
Wanaangamia kutokana na kemeo la uso wako.+
17 Mkono wako na uwe juu yake mtu wa mkono wako wa kuume,+
Juu ya mwana wa binadamu ambaye umemfanya kuwa mwenye nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+
18 Nasi hatutageuka kutoka kwako.+
Utuhifadhi hai, ili tupate kuliitia jina lako.+
19 Ee Yehova Mungu wa majeshi, uturudishe;+
Uutie uso wako nuru, ili tupate kuokolewa.+