1 Wakorintho
16 Basi kuhusu mchango+ ulio kwa ajili ya watakatifu,+ kama vile nilivyoyapa maagizo makutaniko ya Galatia,+ ninyi wenyewe pia fanyeni vivyo hivyo. 2 Kila siku ya kwanza ya juma acheni kila mmoja wenu kwenye nyumba yake mwenyewe aweke kando kitu fulani katika akiba kulingana na anavyofanikiwa, ili nitakapofika michango isifanywe wakati huo. 3 Lakini nitakapofika hapo, watu wowote mtakaokubali kwa barua,+ nitawatuma hao kuipeleka zawadi yenu ya fadhili mpaka Yerusalemu. 4 Hata hivyo, ikiwa inafaa mimi kwenda huko pia, wao wataenda huko pamoja nami.
5 Lakini nitakuja kwenu wakati nitakapokuwa nimekwenda kupitia Makedonia, kwa maana ninaenda kupitia Makedonia;+ 6 na labda nitakaa au hata nitapisha majira ya baridi kali nikiwa pamoja nanyi, ili mnisindikize+ hatua fulani mahali ambapo huenda nitakuwa nikienda. 7 Kwa maana sitaki kuwaona ninyi sasa wakati ninapopita, kwa maana natumaini kukaa pamoja nanyi kwa wakati fulani,+ Yehova+ akiruhusu.+ 8 Lakini ninakaa katika Efeso+ mpaka sherehe ya Pentekoste; 9 kwa maana nimefunguliwa mlango mkubwa unaoongoza kwenye utendaji,+ lakini kuna wapinzani wengi.
10 Hata hivyo, Timotheo+ akifika, hakikisheni kwamba haogopi akiwa kati yenu, kwa maana anafanya kazi ya Yehova,+ kama mimi. 11 Kwa hiyo, mtu yeyote asimdharau.+ Msindikizeni hatua fulani kwa amani, ili anifikie hapa, kwa maana ninamngojea nikiwa pamoja na akina ndugu.
12 Basi kumhusu Apolo+ ndugu yetu, nilimsihi sana aje kwenu akiwa na akina ndugu, na bado hayakuwa mapenzi yake hata kidogo aje sasa; lakini atakuja atakapopata nafasi.
13 Kaeni macho,+ simameni imara katika imani,+ endeleeni kuwa kama wanaume,+ iweni na nguvu.+ 14 Mambo yenu yote na yatendeke kwa upendo.+
15 Sasa nawahimiza ninyi, akina ndugu: Mnajua kwamba nyumba ya Stefana ndiyo matunda ya kwanza+ ya Akaya na kwamba walijitoa kuwahudumia watakatifu.+ 16 Ninyi pia endeleeni kujitiisha kwa watu wa aina hiyo na kwa kila mtu anayeshirikiana na kufanya kazi ya jasho.+ 17 Lakini nashangilia kuwapo kwa Stefana+ na Fortunato na Akaiko, kwa sababu wao wamejazia kutokuwapo kwenu hapa. 18 Kwa maana wameiburudisha roho+ yangu na yenu. Kwa hiyo watambueni watu wa namna hiyo.+
19 Makutaniko ya Asia yanawatumia ninyi salamu+ zao. Akila na Priska pamoja na kutaniko lililo katika nyumba yao+ wanawasalimu ninyi kwa ukunjufu wa moyo katika Bwana. 20 Ndugu wote wanawasalimu ninyi. Salimianeni kwa busu takatifu.+
21 Hii ni salamu yangu, ya Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe.+
22 Ikiwa yeyote hana upendo kwa Bwana, mtu huyo na alaaniwe.+ Uje, Ee Bwana wetu!+ 23 Fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu na ziwe pamoja nanyi. 24 Upendo wangu na uwe pamoja nanyi nyote katika muungano na Kristo Yesu.