Hosea
14 “Ee Israeli, rudi kwa Yehova Mungu wako,+ kwa maana umejikwaa katika kosa lako.+ 2 Chukueni maneno pamoja nanyi mrudi kwa Yehova.+ Mwambieni hivi, enyi nyote, ‘Samehe kosa letu;+ na ukubali lililo jema, nasi tutatoa ng’ombe-dume wachanga wa midomo yetu.+ 3 Ashuru yenyewe haitatuokoa.+ Hatutapanda farasi.+ Na hatutaiambia tena kazi ya mikono yetu: “Ee Mungu wetu!” kwa sababu ni kupitia wewe kwamba mvulana asiye na baba huonyeshwa rehema.’+
4 “Nitaponya ukosefu wao wa uaminifu.+ Nitawapenda kwa kupenda kwangu mwenyewe,+ kwa maana hasira yangu imegeuka kutoka kwake.+ 5 Nitakuwa kama umande kwa Israeli.+ Atachanua kama yungiyungi, na kueneza mizizi yake kama mti wa Lebanoni. 6 Matawi yake yatasambaa, na utukufu wake utakuwa kama ule wa mzeituni,+ na harufu yake nzuri itakuwa kama ile ya mti wa Lebanoni. 7 Watakaa tena katika kivuli chake.+ Watakuza nafaka, nao watachipuka kama mzabibu.+ Ukumbusho wake utakuwa kama divai ya Lebanoni.
8 “Efraimu atasema, ‘Nina nini tena na sanamu?’+
“Hakika mimi mwenyewe nitatoa jibu, nami nitaendelea kumtazama.+ Mimi ni kama mberoshi wenye majani mengi.+ Matunda kwa ajili yako yatapatikana kwangu.”
9 Ni nani aliye na hekima, apate kuelewa mambo haya?+ Mwenye busara, apate kuyajua?+ Kwa maana njia za Yehova zimenyooka,+ na waadilifu ndio watakaotembea katika hizo;+ bali wakosaji ndio watakaojikwaa katika hizo.+