2 Yohana
Barua ya Pili ya Yohana
1 Mwanamume mzee,+ kwa bibi aliyechaguliwa,+ na kwa watoto wake, ambao mimi nawapenda+ kweli, na si mimi peke yangu, bali pia wale wote ambao wameijua kweli,+ 2 kwa sababu ya kweli ambayo inakaa ndani yetu,+ nayo itakuwa pamoja nasi milele.+ 3 Fadhili zisizostahiliwa,+ rehema na amani zitakuwa pamoja nasi kutoka kwa Mungu Baba+ na kutoka kwa Yesu Kristo Mwana wa Baba, pamoja na kweli na upendo.+
4 Ninashangilia sana kwa sababu nimekuta baadhi ya watoto+ wako wanatembea katika kweli,+ kama vile tulivyopokea amri kutoka kwa Baba.+ 5 Basi sasa ninakuomba, Ee bibi, kama mtu anayekuandikia, si amri+ mpya, bali ambayo tulikuwa nayo tangu mwanzo,+ kwamba tupendane.+ 6 Na upendo unamaanisha hivi,+ kwamba tuendelee kutembea kulingana na amri+ zake. Hii ndiyo amri, kama vile mlivyosikia tangu mwanzo, kwamba mnapaswa kuendelea kutembea ndani yake.+ 7 Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea katika ulimwengu,+ watu ambao hawamkiri Yesu Kristo kuwa alikuja katika mwili.+ Hao ndio yule mdanganyifu+ na mpinga-Kristo.+
8 Jihadharini, msije mkapoteza mambo ambayo sisi tumefanya kazi ili kuyatokeza, bali mpate thawabu kamili.+ 9 Kila mtu anayevuka mipaka+ naye hakai+ katika fundisho la Kristo hana Mungu.+ Yeye ambaye anakaa katika fundisho hili ndiye aliye na Baba na Mwana pia.+ 10 Mtu yeyote akija kwenu naye haleti fundisho hili, msimpokee kamwe nyumbani+ mwenu wala kumsalimu.+ 11 Kwa maana yeye anayemsalimu anashiriki katika matendo yake maovu.+
12 Ijapokuwa nina mambo mengi ya kuwaandikia ninyi, sitaki kufanya hivyo kwa karatasi na wino,+ lakini ninatumaini kuja kwenu na kusema nanyi uso kwa uso,+ ili shangwe+ yenu iwe kamili.+
13 Watoto wa dada yako, yule aliyechaguliwa, wanakutumia salamu+ zao.