99 Yehova amekuwa mfalme.+ Vikundi vya watu na vifadhaike.+
Anaketi juu ya makerubi.+ Dunia na itetemeke.+
2 Yehova ni mkuu katika Sayuni,+
Naye yuko juu ya vikundi vyote vya watu.+
3 Na walisifu jina lako.+
Ni kuu na lenye kuogopesha, ni takatifu.+
4 Na kwa nguvu za mfalme ameipenda hukumu.+
Wewe mwenyewe umeufanya imara unyoofu.+
Umetekeleza hukumu na uadilifu katika Yakobo.+
5 Mtukuzeni Yehova Mungu wetu+ na kuinama chini penye kiti cha miguu yake;+
Yeye ni mtakatifu.+
6 Musa na Haruni walikuwa kati ya makuhani wake,+
Na Samweli alikuwa kati ya wale walioliitia jina lake.+
Walikuwa wakimwita Yehova, naye akaendelea kuwajibu.+
7 Katika nguzo ya wingu aliendelea kusema nao.+
Walishika vikumbusho vyake na sharti alilowapa.+
8 Ee Yehova Mungu wetu, wewe mwenyewe uliwajibu.+
Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe,+
Na mwenye kulipiza kisasi juu ya matendo yao yenye sifa mbaya.+
9 Mtukuzeni Yehova Mungu wetu+
Na mwiname kwenye mlima wake mtakatifu.+
Kwa maana Yehova Mungu wetu ni mtakatifu.+