Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 30:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Yehova Mungu wenu atawarudisha katika nchi ambayo baba zenu walimiliki, nanyi mtaimiliki; naye atawafanikisha na kuwafanya mwongezeke kuliko baba zenu.+

  • Isaya 65:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Watajenga nyumba na kuishi ndani yake,+

      Nao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.+

  • Yeremia 32:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Nyumba na mashamba na mashamba ya mizabibu yatanunuliwa tena katika nchi hii.’”+

  • Ezekieli 28:25, 26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 “‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Nitakapowakusanya tena watu wa nyumba ya Israeli kutoka miongoni mwa mataifa walikotawanywa,+ nitatakaswa kati yao machoni pa mataifa.+ Nao watakaa katika nchi yao+ niliyompa mtumishi wangu Yakobo.+ 26 Wataishi huko kwa usalama+ na watajenga nyumba na kupanda mashamba ya mizabibu+ na watakaa kwa usalama nitakapotekeleza hukumu dhidi ya wote wanaowazunguka ambao wanawadhihaki;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao.”’”

  • Amosi 9:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Nitawakusanya na kuwarudisha watu wangu Waisraeli walio utekwani,+

      Nao watajenga upya majiji yaliyoachwa ukiwa na kuishi humo;+

      Watapanda mashamba ya mizabibu na kunywa divai yake,+

      Nao watalima bustani za matunda na kula matunda yake.’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki