96 Mwimbieni Yehova wimbo mpya.+
Mwimbieni Yehova, dunia yote!+
 2 Mwimbieni Yehova; lisifuni jina lake.
Tangazeni habari njema za wokovu wake siku baada ya siku.+
 3 Tangazeni utukufu wake miongoni mwa mataifa,
Kazi zake zinazostaajabisha miongoni mwa mataifa yote.+
 4 Yehova ni mkuu na anastahili kusifiwa kuliko wote.
Anaogopesha kuliko miungu mingine yote.
 5 Miungu yote ya mataifa ni miungu ya ubatili,+
Lakini Yehova ndiye aliyeziumba mbingu.+
 6 Mbele zake kuna utukufu na fahari;+
Nguvu na uzuri umo mahali pake patakatifu.+
 7 Mpeni Yehova anachostahili, enyi familia za mataifa,
Mpeni Yehova anachostahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+
 8 Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili;+
Leteni zawadi na mwingie katika nyua zake.
 9 Mwinamieni Yehova katika mapambo matakatifu;
Tetemekeni mbele zake, dunia yote!
10 Tangazeni miongoni mwa mataifa: “Yehova amekuwa Mfalme!+
Dunia imeimarishwa kabisa, haiwezi kusogezwa.
Atayahukumu mataifa kwa haki.”+
11 Mbingu na zishangilie, dunia na iwe na shangwe;
Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza;+
12 Mashamba na vitu vyote vilivyomo na vishangilie.+
Wakati uleule miti yote ya msituni na ishangilie kwa sauti+
13 Mbele za Yehova, kwa maana anakuja,
Anakuja kuihukumu dunia.
Ataihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa+
Na mataifa kwa uaminifu wake.+