96 Mwimbieni Yehova wimbo mpya.+
Mwimbieni Yehova, enyi watu wote wa dunia.+
2 Mwimbieni Yehova, libarikini jina lake.+
Tangazeni habari njema za wokovu wake siku baada ya siku.+
3 Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa,+
Kazi zake za ajabu kati ya vikundi vyote vya watu.+
4 Kwa maana Yehova ni mkuu+ na wa kusifiwa sana.
Ni mwenye kuogopesha kuliko miungu mingine yote.+
5 Kwa maana miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu isiyo na thamani;+
Lakini Yehova, amezifanya mbingu.+
6 Utukufu na fahari ziko mbele zake;+
Nguvu na uzuri zipo katika patakatifu pake.+
7 Mhesabieni Yehova, enyi familia za vikundi vya watu,+
Mhesabieni Yehova utukufu na nguvu.+
8 Mhesabieni Yehova utukufu wa jina lake;+
Chukueni zawadi na mwingie katika nyua zake.+
9 Mwinamieni Yehova katika pambo takatifu;+
Iweni na maumivu makali kwa sababu yake, enyi nyote watu wa dunia.+
10 Semeni kati ya mataifa: “Yehova amekuwa mfalme.+
Nchi yenye kuzaa pia hufanywa imara ili isitikiswe.+
Yeye atatetea kwa unyoofu vikundi vya watu katika kesi yao.”+
11 Mbingu na zifurahi, na dunia ishangilie.+
Bahari na ingurume na vitu vinavyoijaza.+
12 Nchi na ifurahi na vyote vilivyomo.+
Na wakati uleule miti yote ya msituni na ishangilie+
13 Mbele za Yehova. Kwa maana amekuja;+
Kwa maana amekuja kuihukumu dunia.+
Ataihukumu kwa uadilifu nchi yenye kuzaa+
Na vikundi vya watu kwa uaminifu.+